“Njia 5 za Kushughulikia Hisia Kubwa,” Rafiki, Machi 2025, 38–39.
Njia 5 za Kushughulikia Hisia za Huzuni
Maisha yanaweza kuwa magumu wakati mwingine! Kuhisi hisia nyingi, kama huzuni na wasiwasi, ni sehemu ya uzoefu wetu wa kuishi duniani.
Katika maandiko, tunajifunza kwamba hata Mwokozi alihisi huzuni wakati mwingine pia (ona Yohana 11:32–36). Yesu Kristo aliteseka aina zote za maumivu. Kwa sababu ya hili, Yeye anajua hasa jinsi unavyohisi. Yeye pia anajua hasa jinsi ya kukusaidia. (Ona Alma 7:11–12.)
Hapa kuna mambo matano ya kukusaidia wakati unapohisi kuvunjika moyo.
1
Sali kwa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya msaada.
Unaposali kwa ajili ya msaada, Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanaweza kukuongoza (ona Alma 37:36–37). Wanakupenda, na wanataka kukusaidia.
2
Kumbuka kwamba wewe unapendwa.
Maandiko yanafundisha kwamba “thamani ya nafsi ni kubwa mbele za Mungu” (Mafundisho na Maagano 18:10). Hiyo inamaanisha kuwa unapendwa na wewe ni muhimu kwa Baba wa Mbinguni!
3
Nenda nje!
Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo waliumba ulimwengu huu mzuri kwa ajili yetu. Kucheza nje kunakusaidia kuwa na afya na nguvu, na inaweza pia kukusaidia kujisikia vizuri zaidi na kutulia zaidi.
4
Andika jinsi unavyohisi.
Kutunza shajara kunaweza kukusaidia kukumbuka masomo unayojifunza katika maisha. Inaweza pia kukusaidia kuelewa vyema kile unachohisi.
5
Zungumza na mtu mzima unayemwamini.
Unapozungumza na mtu kuhusu jinsi unavyohisi, wanaweza kusaidia kukukumbusha jinsi ulivyo maalumu. Wanaweza pia kukusaidia kujua jinsi ya kupata msaada unaouhitaji.
Wakati mwingine, hata baada ya kufanya mambo haya, unaweza bado kuhisi huzuni. Unaweza kuhitaji kuzungumza na daktari ili kukusaidia kuhisi vizuri zaidi. Na unaweza daima kuomba baraka ya ukuhani. Bila kujali chochote, hauko peke yako! Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanakupenda. Wanataka kukubariki na kukusaidia.
Vielelezo na Stephanie Mackay