“Halo kutoka Madagaska!” Rafiki, Machi 2025, 8–9.
Halo kutoka Madagaska!
Madagaska ni nchi iliyoko katika pwani ya mashariki ya kusini mwa Afrika. Karibia watu milioni 30 wanaishi huko. Lugha zao rasmi ni Kimalagasi na Kifaransa.
Imezungukwa na Maji
Madagaska ni kisiwa cha nne kwa ukubwa zaidi duniani.
Maumbo ya Mawe
Hifadhi ya Taifa ya Tsingy de Bemahara ina misitu ya mawe iliyotengenezwa kwa chokaa. Baadhi ya maumbo yana futi 328 (mita 100) kwa urefu!
Kutengeneza Vanilla
Madagaska inakuza vanilla ambayo inauzwa duniani kote. Nchi inazalisha takribani tani 3,300 (tani za mita 3,000) za vanilla kwa mwaka!
Mti wa Mbuyu
Mbuyu ni mti wa kitaifa wa Madagaska na unaweza kuishi kwa zaidi ya miaka 1,000. Mti wa mbuyu huwapa watu matunda ya kula, ganda la kutengenezea kamba, na kinga dhidi ya jua.
Wanyama Maalum
Kuna aina nyingi tofauti za komba. Wote wanatoka Madagaska.
Mnyama mwingine kutoka nchi hii ni zebu, ambayo ni aina ya ng’ombe ambao watu huwatumia kwa ajili ya kulima, maziwa, na kusafiri.