“Msaada kutoka Mbinguni,” Rafiki, Machi 2025, 20–21.
Msaada kutoka Mbinguni
Imetoholewa kutoka kwa “Je, Unataka Kuwa na Furaha?” Liahona, Nov. 2023, 46–48.
Niliitwa kuwa askofu katika wakati mgumu katika maisha yangu. Nilikuwa baba kijana mwenye familia, na tulikuwa tukihangaika sana kupata pesa. Nilikuwa nimechoka. Ilikuwa vigumu pia kwa mke wangu.
Jumapili moja mke wangu mpendwa alikuwa akipokea sakramenti. Roho alimsaidia kutambua kitu fulani. Matatizo mengi tuliyokumbana nayo yalitatuliwa wakati fulani wa wito wangu.
Bwana anayajua mahitaji yetu. Yeye anapotuomba kutumikia, Anajua kile kitakachotusaidia sisi zaidi. Yeye anataka kutubariki. Na Yeye atatupa baraka hizi tunapomtumikia kwa uaminifu.
Je, unataka kuwa na furaha? Baki katika njia ya agano. Mwokozi wetu anatualika tuje Kwake. Yeye anabeba mizigo yetu. Yesu Kristo hufanya maisha yetu kuwa rahisi na yenye furaha zaidi. Na Yeye hutujaza na shangwe.
Muda wa Usaili!
Muulize mwanafamilia kuhusu jinsi Baba wa Mbinguni alivyowabariki. Hapa kuna baadhi ya maswali ya kukuwezesha kuanza:
-
Je, unaweza kuniambia kuhusu wakati ambapo Baba wa Mbinguni aliibariki familia yetu?
-
Ni kwa jinsi gani unapenda kuwasaidia wengine? Ni baraka zipi umeziona wakati ulipowatumikia wengine?
-
Je, ni kwa nini unamfuata Yesu Kristo? Ni kwa jinsi gani kumfuata Yeye kumekusaidia kuwa na furaha?`
Vielelezo na Turine Tran