2025
Shughuli ya 99+1 ya Historia ya Familia, Kata ya Nairobi 2nd
Januari 2025


Kurasa za Karibu

Shughuli ya 99+1 ya Historia ya Familia, Kata ya Nairobi 2nd

Urais wa Eneo la Afrika ya Kati ulizihimiza kata zote katika Eneo kuwasilisha majina 99+1 kwenye FamilySearch katika kusherehekea Siku ya Kuzaliwa ya Kuzaliwa ya miaka 100 ya Rais Nelson.

Katika kata ya Nairobi 2nd, Askofu Kennedy Mukula aliichukua changamoto hii, kwa kupanga shughuli ya kata kwa ajili ya Agosti 31, siku kumi tu kabla ya tukio la nabii la miaka 100.

Kukusanya majina kungehitaji kompyuta nyingi, na baadhi ya wataalamu wa historia ya familia. Eric Onyango, Rais wa Akidi ya Wazee na mhandisi mtaalamu wa mtandao, ambaye pia alihudumu kama Mshauri wa Eneo wa Historia ya Familia, aliombwa kutoa teknolojia. Wamisionari wanandoa wanaohudumu katika kata, Mzee na Dada Arrington, waliombwa kuwasaidia waumini kuingiza majina.

“Tulitaka kuhakikisha watu walikuwa na njia ya kukusanya majina na tarehe za kuzaliwa,” Mzee Arrington alisema, “hivyo basi tulitengeneza fomu rahisi ambayo waumini wangekwenda nayo nyumbani na kuitumia kukusanya majina kutoka kwa familia zao. Tuligawa fomu hizi kanisani katika Jumapili mbili kabla ya shughuli hii. Na watu walikuja wakiwa wamejiandaa!”

“Hatukuwa na uhakika ni kompyuta nyingi kiasi gani tungehitaji, lakini tulileta zile tulikuwa nazo,” alisema Askofu Mukula. “Uaskofu kila mmoja alileta moja, akina Arrington walileta tatu, na Eric alileta 5 zaidi. Mwishoni, bado tulikuwa na watu wakingojea kwenye foleni ili kuongeza majina yao.”

Lengo lilikuwa kufikisha au kuzidi majina 99+1 ya familia kuingizwa katika familysearch.org, kwa hiyo kufuatilia kulikuwa muhimu kwa kata.

“Tulitengeneza kadi za majina kwa kuchapisha ikoni za watu zinazofanana na zile zilizo ndani ya familysearch takribani sentimita 10 za mraba,” alisema Dada Arrington. “Kisha tuliwaomba waumini kuandika jina moja ambalo waliliongeza katika familysearch kwenye kila karatasi na kuibandika kwenye ubao mweupe ili tuweze kuhesabu. Tulikuja na karatasi tupu za ikoni 140, na ziliisha hata kabla ya shughuli kuisha. Waumini walikuwa wakiandika majina manne, matano, au sita kwenye karatasi moja ya ikoni!”

“Kila mtu alikuwa akifanya kazi ya kuingiza majina, na niliipenda.” Alisema Beatrice Kiragu, mshauri wa kwanza katika Muungano wa Usaidizi wa kata. “Nilipenda hisia ya kuingiza majina, lakini zaidi nilifurahia kuwaanda mababu zangu kwa ajili ya baraka za hekaluni.”

Wengi wa waumini waliokuwa wanahudhuria walipata kwenda nyumbani na kumbukumbu maalumu. Walijaza mti maalumu wa Kiafrika kwa majina ya familia zao, na karani wa kata alichapisha moja kwa kila familia kwenye karatasi ya ubora wa picha.

Mercy Kinyaka, Katibu wa Muungano wa Usaidizi wa kata, alifurahi kupata hata wengi wa familia yake wakiwa tayari mtandoani. “Niliingiza majina machache, kisha FamilySearch iliniunganisha na sehemu ya familia yangu iliyokuwa tayari kwenye mfumo. Nilikuwa na furaha sana! Huo ni mti wangu wa familia!”

Askofu Mukula alifurahishwa na matokeo. Wakati shughuli ikikaribia kuisha, zaidi ya majina 200 mapya ya familia yalikuwa yameingizwa katika familysearch.org.

Dada Arringtons anakumbuka, “Tuliishia kuchelewa sana kwa sababu watu bado walikuwa na majina ya kuingiza. Mshiriki wetu wa mwisho alikuwa si muumini. Tulitazama alipokuwa akiingiza majina 15 kutoka kwa familia yake. Alikuwa na furaha sana kupokea picha ya mti wake mwenyewe wa familia!”

Askofu Mukula alielezea furaha ambayo waumini wengi waliihisi “wakati mioyo yao ilipowageukia baba zao! Na tulipenda kumsaidia Rais Nelson kusherekea siku yake ya kuzaliwa!”