2025
Kanisa la Yesu Kristo la Urejesho
Januari 2025


“Kanisa la Yesu Kristo la Urejesho,” Liahona, Jan. 2025.

Kutumia Majarida ya Kanisa

Kanisa la Yesu Kristo la Urejesho

familia nje ya hekalu

Mafunzo ya Njoo, Unifuate ya mwaka huu ya Mafundisho na Maagano yataonyesha jinsi Bwana alivyorejesha Kanisa Lake na injili Yake kupitia manabii wa siku za mwisho. Makala nyingi katika toleo la mwezi huu zinaonyesha baraka za Urejesho.

Kujifunza kutoka kwenye Toleo Hili

Shiriki katika Kukusanyika.

Kwenye ukurasa wa 2, Rais Russell M. Nelson anashiriki njia tunavyoweza kukusanyika kwa Mwokozi, kukusanyika na Watakatifu, na kukusanyika katika huduma ya Mungu. Fikiria kuweka lengo la mwezi huu ili kuchangia mojawapo ya aina hizo tatu za kukusanyika.

Tumikia katika Kanisa la Urejesho

Mzee Patrick Kearon wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili anazungumza kuhusu fursa tulizonazo katika Kanisa la Yesu Kristo la urejesho za “kuwatumikia wengine kwa upendo” (ona ukurasa wa 8). Je, kuna watu katika kata au tawi lako ambao wanasumbuka? Ungeweza kuwaombea watu hawa na kuomba mwongozo wa kiungu juu ya jinsi ya kuwahudumia.

Jifunze kutoka kwenye Tangazo la Urejesho

Mnamo 2020, Urais wa Kwanza na Akidi ya Mitume Kumi na Wawili walitoa “Urejesho wa Utimilifu wa Injili ya Yesu Kristo: Tangazo kwa Ulimwengu la Miaka Mia Mbili” (ona ukurasa wa 40). Unaporejelea tangazo la Urejesho, unaweza kufikiria maswali haya: Ni matukio gani muhimu yanayotajwa, na ni kwa jinsi gani Bwana aliongoza matukio hayo?