2025
Kukumbuka Kwa Nini Ninaishi Injili
Januari 2025


“Kukumbuka Kwa Nini Ninaishi Injili,” Liahona, Jan. 2025.

Vijana Wakubwa

Kukumbuka Kwa Nini Ninaishi Injili

Kujikumbusha kuhusu “kwa nini” yangu kunakonitia motisha kusogea karibu na Mwokozi na kufuatilia malengo yangu ya kiroho.

msichana mtu mzima akisali

Maisha yangu yanahisi kuwa na vurugu wakati mwingine, lakini ninapenda faraja ninayohisi ninapotembea kwenda kanisani. Ni moja ya sababu ya kwa nini ninapenda kwenda kanisani!

Na ninapokumbuka kile ninachopenda kuhusu injili—kama vile kuhisi Roho Mtakatifu, kwa mfano—ninahisi msukumo wa kufuatilia zaidi tabia zangu za kiroho, kama kwenda hekaluni, kusoma maandiko yangu, na kuomba kwa Baba wa Mbinguni.

Kwa sababu maisha yanaweza kuwa na shughuli nyingi, inaweza kuwa rahisi kusahau vitu hivi rahisi tunavyopenda. Lakini mara kwa mara kujikumbusha mwenyewe sababu za kwa nini ninaishi na kupenda injili ya Yesu Kristo hunisaidia kufanya upya malengo yangu ya kiroho ambayo yatanileta karibu Naye na Baba wa Mbinguni.

Kuweka Malengo Mapya ya Kiroho

Mwanzoni mwa kila mwaka, ninapenda kutathmini upya malengo yangu ya kiroho kwa kuandika maazimio ya Mwaka Mpya. Ikiwa pia unafanya tafakuri ndogo na kufikiria jinsi unataka kuboresha uhusiano wako na Kristo katika mwaka huu mpya, jiulize swali hili:

“Kwa nini ninapenda injili ya Yesu Kristo?”

Dada Ann M. Dibb, Mshauri wa Pili wa zamani katika Urais Mkuu wa Wasichana, alieleza kwamba “upendo wetu kwa injili unakua tunapopata uzoefu wa upendo wa Baba yetu wa Mbinguni na amani iliyoahidiwa na Mwokozi tunapomwonyesha kuwa tuko tayari kumtii na kumfuata Yeye.”

Kujua kwa nini unaipenda injili kutakusaidia kuhisi na kutambua upendo ambao Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanao kwa ajili yako. Mawazo haya pia yatakusaidia kuhisi kidogo kutokuzidiwa wakati unapojitahidi kuweka na kufikia malengo yako ya kiroho.

“Kwa nini” yangu kwa kuishi na kuipenda injili ya Yesu Kristo inajumuisha ufahamu kwamba familia zinaweza kuwa pamoja milele na amani ninayoihisi baada ya sala ya unyenyekevu kwa Baba wa Mbinguni.

Bila kujali “kwa nini” yako ni ipi, ishikilie—itakupa msukumo wa kasi ya kiroho unaohitaji kuwa mwanafunzi bora wa Yesu Kristo.

Kuishi “Kwa nini” Yako

Mara nilipotambua kwa nini nilikuwa nikiishi injili, jinsi nilivyoendelea kuweka malengo yangu ya kiroho kulibadilika. Niliacha kufikiria kuhusu kile nilichokuwa nikishindwa kufanya na nikawa nimefokasi zaidi kwenye kile ambacho ningeweza kufanya. Nilikumbuka kwamba ninaishi injili kwa sababu ninampenda Mwokozi wangu.

Mzee Dieter F. Uchtdorf wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alisema: “Tunahitaji kukubali kwamba amri za Mungu sio tu orodha ndefu ya mawazo mazuri. … Ni ushauri mtukufu, ulio na msingi kwenye kweli za milele, uliotolewa ili kuleta ‘amani katika ulimwengu huu, na uzima wa milele katika ulimwengu ujao’ [Mafundisho na Maagano 59:23].”

Kufuatilia malengo yangu ya kiroho kunanikumbusha mimi ni nani: mtoto mtukufu wa wazazi wa mbinguni. Kanuni hiyo inanipa ujasiri wa kukabiliana na wasiwasi na udhaifu wangu kupitia Yesu Kristo (ona Etheri 12:27).

Rais Russell M. Nelson, alifundisha kwamba “Bwana hatarajii ukamilifu kutoka kwetu kwenye hatua hii ya ukuaji wetu wa milele. Lakini anatarajia sisi tuongezeke katika kuwa wasafi.” Kwa hiyo ninajaribu kadiri niwezavyo kila siku kubaki karibu na Yesu Kristo na kukumbuka kwa nini ninachagua kumfuata Yeye.