UrejeshoUnaoendelea
Ukengeufu Mkuu
Vielelezo na Katy Dockrill
Watu wanageuka dhidi ya Mwokozi na Mitume Wake. Kanisa linaanguka kwenye uharibifu wa kiroho na halipo tena duniani.
1820
Ono la Kwanza Mungu Baba na Yesu Kristo wanamtokea Joseph Smith mwenye umri wa miaka 14.
1823
Malaika Moroni anamtokea Joseph Smith, akimwambia kuhusu mabamba ya dhahabu.
1829–1830
Ukuhani wa Haruni na Ukuhani wa Melkizedeki unarejeshwa.
Joseph Smith anatafsiri Kitabu cha Mormoni (karibu ndani ya miezi mitatu!), na kinachapishwa.
Kanisa linaanzishwa rasmi, mnamo Aprili 6, 1830.
waumini rasmi 6 wa mwanzo; punde baadaye, 280
1835–1836
Akidi ya Mitume Kumi na Wawili inaanzishwa
Kitabu cha Mafundisho na Maagano kinachapishwa
Mwokozi, Musa, Elia, na Eliya wanatokea katika Hekalu la Kirtland na kurejesha funguo za ukuhani (ona Mafundisho na Maagano 110).
Zaidi ya waumini 13,000
Hekalu 1
1840–1842
Ubatizo kwa niaba ya wafu unafundishwa hadharani.
Muungano wa Usaidizi unaanzishwa.
Endaumenti kamili ya kwanza ya hekaluni inatolewa.
1869–1880
Programu za Wasichana na Wavulana za mwanzo zinaanzishwa.
Kitabu cha Lulu ya Thamani Kuu kinakubaliwa kama kitabu kitakatifu.
Zaidi ya waumini 133,000
Hekalu 1
1936
Programu ya awali ya ustawi wa Kanisa inaanza.
Zaidi ya waumini 760,000
Mahekalu7
1978
Ibada za hekaluni zinazotolewa kwa waumini watu wazima wote wenye kustahili, na kutawazwa katika ukuhani kwa wanaume wote wenye kustahili kunaidhinishwa.
Zaidi ya waumini milioni 4
Mahekalu 17, ikijumuisha Uswisi, New Zealand, Uingereza, na Brazil
1995
“Familia: Tangazo kwa Ulimwengu linatolewa.
Zaidi ya waumini milioni 9.25
Mahekalu 47, yaliyotawanyika zaidi ya mabara 6
2012
Umri wa misheni umeshushwa kutoka 19 hadi 18 kwa wanaume na kutoka 21 hadi 19 kwa wanawake.
Zaidi ya waumini milioni 14.5
Mahekalu 140
2018–2020
Vijana wanapewa fursa pana za kuhudumu hekaluni.
Ratiba ya Kanisa Jumapili inafupishwa kutoka masaa 3 hadi 2.
Zaidi ya waumini milioni 16.5
Mahekalu 168
2025
Urejesho bado unaendelea! Kuna waumini wa Kanisa katika zaidi ya nchi na mipaka ya kijiografia 200, wakizungumza zaidi ya lugha 700!
Kuanzia Aprili 2024: mahekalu 189 yaliyowekwa wakfu, 161 zaidi yalitangazwa (jumla 350).
Zaidi ya waumini milioni 17.25