Kushughulikia Maswali Yangu kuhusu Historia ya Kanisa
Ingawa nilikuwa na maswali, sikukata tamaa au kukubali kushindwa.
Katika darasa langu la historia, mwalimu wangu alianza kuzungumza kuhusu Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. Hakuwa na maoni makubwa juu ya Kanisa. Alisema tulikuwa waamini wa ndoa za mitala na wabaguzi.
Kila kitu nilichojifunza hapo awali kuhusu Kanisa kilikuwa na maana kwangu. Lakini uzoefu wangu darasani ulinifanya nifikirie kuhusu baadhi ya maswali magumu kutoka kwenye historia ya Kanisa, kama vile kwa nini watu weusi hawakuruhusiwa kushikilia ukuhani kwa muda, na kwa nini ndoa za mitala zilitokea.
Kwa sababu hiyo, nilianza kufikiria, kutafakari, na kuomba. Nilisoma kutoka kwenye maandiko, nikaongea na wazazi wangu na viongozi, na kujifunza zaidi mimi mwenyewe. Ingawa nilikuwa na maswali, sikukata tamaa au kukubali kushindwa.
Nilipojifunza na kusoma, nilihisi kama nilikuwa nabebwa. Bado sielewi kila kitu, lakini niliweza kupata amani.
Sasa ninapokuwa na maswali, ninashikilia kile ambacho tayari ninakijua, kama uzoefu wote ambao umesaidia ushuhuda wangu kukua. Wakati kitu kinaponishinda, sala kwa kawaida ndiyo suluhisho langu, na kisha ninajaribu kumsikiliza Roho wakati ninaposoma maandiko.
Mwaka huu uliopita, kwa kweli nimekuja kujua nguvu ya Roho, na nimehisi amani na faraja na upendo. Ninajua kwamba kuna Mungu anayezungumza nasi na anataka sisi turudi nyumbani.
Mwandishi anaishi Texas, Marekani.