Sauti za Vijana
Rafiki Bora wa Kweli
Joel A., miaka 19, Yerevan, Armenia
Anapenda kufanya sanaa, kusanidi programu, na kujifunza ujuzi mpya, kama vile kupika.
Nilikuwa na marafiki kadhaa ambao walinigeuka kati ya kipindi cha darasa la saba na la tisa. Mwanzoni sikutambua kwamba walikuwa wakinidhihaki, lakini nilipotambua hilo, nilishtuka na sikuweza kuelewa wapi nimekosea.
Nilifikiria kwamba kama ningefanya kile ambacho Kristo angefanya, kila kitu kingeenda vyema. Kwa hivyo niliendelea kuwa mwema, nikiwasaidia wanadarasa wenzangu katika kazi zao za nyumbani, na kumtegemea Mungu, nikiamini kwamba siku moja ningepata rafiki mwema. Mwanzoni, si mengi yalionekana kubadilika. Lakini baada ya kuanza shule ya upili, wanadarasa wenzangu walikuwa watu wazuri zaidi.
Muhimu zaidi, katika miaka hiyo wakati nilipokuwa nikitafuta marafiki, niligundua kwamba rafiki yangu mkubwa ni Yesu Kristo. Kwa hiyo siyo tu nilipata marafiki wapya shuleni, lakini pia niltengeneza Rafiki aliye bora zaidi ambaye ningeweza kuwa naye.