“Kujenga Nauvoo,” Rafiki, Septemba 2025, 26–28.
Hadithi za Maandiko
Kuijenga Nauvoo
Bwana aliwaambia Watakatifu kukusanyika katika sehemu mpya. Ilikuwa karibu na mto mkubwa, ambapo nchi ilikuwa imelowa maji na matope. Haikuonekana kama mahali pazuri pa kujenga mji. Lakini Nabii Joseph Smith alijua kwamba kwa msaada wa Bwana, wangeweza kuifanya iwe nzuri.
Watakatifu walifanya kazi kwa bidii ili kupafanya mahali pazuri pa kuishi. Joseph aliuita mji wa Nauvoo, ambao unamaanisha “mahali pazuri.”
Bwana alitaka Watakatifu Wake kujenga hekalu huko Nauvoo. Watu haraka walianza kufanya kazi.
Bwana alikuwa na baraka kuu za kuwapa watu Wake. Hekaluni, wangefanya maagano, au ahadi maalumu, na Bwana. Pia wangejifunza kuhusu mpango wa furaha wa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya watoto Wake wote.
Watakatifu walifanya kazi kwa bidii ili kujenga hekalu. Ilichukua muda mrefu, lakini walikuwa na shauku ya kujifunza kuhusu ahadi maalumu ambazo Bwana alikuwa nazo kwa ajili yao katika hekalu Lake.