2025
Bwana Hakika Anaharakisha Kazi Yake
Novemba 2025


14:55

Bwana Hakika Anaharakisha Kazi Yake

Bwana anapoharakisha kazi Yake, tunapaswa kuwapenda, kuwalea, na kuwatumikia wale wanaokubali injili Yake.

Charles Dickens alianzisha riwaya yake ya kitambo Hadithi ya Miji Miwili kwa madai kwamba “zilikuwa nyakati bora zaidi; zilikuwa nyakati mbaya zaidi.” Kwa maana fulani hii ni kweli katika siku zetu.

Tunaishi katika wakati wenye msukosuko ambapo “dunia yote [iko] katika machafuko.” Wasaa wa Rais Russell M. Nelson wa kuwa wapatanishi, kama wafuasi wa Yesu Kristo, ulisisitizwa vizuri sana asubuhi ya leo na Mzee Gary E. Stevenson. Hii sehemu muhimu ya kujenga umoja, amani, na uponyaji kwa ajili ya “nyakati mbaya zaidi.”

Sisi pia tunaishi katika “nyakati bora zaidi,” ambazo zitakuwa msisitizo wangu. Bwana, katika dibaji ya Mafundisho na Maagano, sehemu ya 1, alitangaza, utimilifu wa injili “utatangazwa … hata miisho ya ulimwengu.” Bwana kwa kweli anaharakisha kazi Yake katika wakati wetu. Tunapaswa kushukuru sana kwa uharakishaji, ambao umeshatokea na unatokea licha ya nyakati hizi zenye changamoto. Tunaishi katika siku ambayo wafuasi wa Bwana wanabahatika kusikia sauti Yake na kuitikia kwa mioyo na akili iliyo wazi. Waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, ambao wamejitolea kwa Mwokozi na amri Zake, wanapata kusudi na amani kuu ya kibinafsi.

Katika nyakati mbalimbali katika historia ya Kanisa, kumekuwa na ongezeko kubwa la wale ambao wameingia katika njia ya agano. Kipindi kimoja kama hicho kilitokea kati ya 1837 na 1850. Baadhi ya Mitume wa mapema katika Kanisa la Bwana lililorejeshwa walihudumu misheni nchini Uingereza. Misheni hizi zilisababisha maelfu kujiunga na Kanisa, na kufikia 1850 kulikuwa na waumini wengi wa Kanisa wanaoishi nchini Uingereza kuliko Marekani. Wakati huo, Bwana aliwaelekeza Watakatifu hawa kukusanyika Utah. Uhamaji wa watu wengi ulitokea, baadhi yao wakiungwa mkono na mikopo ilitolewa kupitia Mfuko wa Kudumu wa Kuhama.

Ninapenda maelezo ya kuwasili huko Salt Lake Valley kwa idadi kubwa ya waongofu kutoka Uingereza na Wales mnamo 1852. Kikundi hicho kilikutana na Urais wa Kwanza kwenye kinywa cha Emigration Canyon, ukiandamana na Bendi ya Kapteni Pitt. Deseret News liliwaeleza kuwa “kundi la walowezi [wakiwemo] akina dada na watoto, wanaotembea, kuchomwa na jua, na kupigwa na hali ya hewa, lakini hawakukata tamaa; mioyo yao ilikuwa miepesi na yenye kuchangamka, jambo lililodhihirishwa waziwazi na nyuso zao zenye furaha na shangwe.”

“Walipopita Uwanja wa Hekalu, … maelfu ya wanaume, wanawake, na watoto, wakikusanyika, kutoka sehemu mbalimbali za jiji, kuungana katika makaribisho matukufu na ya furaha.” Rais Brigham Young aliwahutubia: “Bwana Mungu wa Israeli na awabariki. … Tumewaombeeni daima; maelfu ya maombi yametolewa kwa ajili yenu, siku baada ya siku, kwa Yeye aliyetuamuru tuwakusanye Israeli, tuwaokoe wana wa watu kwa kuhubiri injili, na kuwatayarisha kwa ujio wa Masiya.”

Katika roho ya tukio hilo la furaha, acha niwahakikishie tena waongofu wote wapya na wale wanaorudi katika Kanisa la Bwana: Sisi tunawapenda; tunawahitaji; Bwana anawahitaji. Tunaweza tusikaribishwe na bendi ya kutembea, lakini tunaomba baraka za mbinguni zitashughulikia juhudi zenu za kuendelea katika njia ya agano inayoongoza kwa Mungu Baba na Yesu Kristo katika ufalme wa selestia.

Kuna uthibitisho wazi kwamba imani katika Yesu Kristo inaongezeka katika siku zetu. Katika Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, kumekuwa na ongezeko la ajabu la wongofu na ushiriki wa waongofu. Katika miezi 36 iliyopita karibu waongofu 900,000 wamejiunga na Kanisa. Waongofu hawa wanajumuisha takriban asilimia 5 ya jumla ya waumini wa Kanisa. Tunawakaribisha waumini wapya kwa mikono miwili na shukrani za kina kwa njia mliyochagua.

Waongofu hawa 900,000 katika muda wa miezi 36 iliyopita walizidi jumla ya washiriki wa Kanisa katika maadhimisho yake a 110 katika 1940, ambao walikuwa zaidi ya waumini 860,000. Huu ulikuwa mwaka ambao Mzee Jeffrey R. Holland, Mzee Dieter F. Uchtdorf, na mimi tulizaliwa.

Waongofu hawa wapya wa ajabu wanatoka kila sehemu ya dunia. Katika miezi sita ya kwanza ya mwaka huu, watu walioongoka wameongezeka kwa zaidi ya asilimia 20 kuliko mwaka uliopita katika Ulaya, Afrika, Asia, Pasifiki, na Amerika Kusini. Nchini Amerika Kaskazini tumeona ongezeko la asilimia 17. Kazi ya Bwana inaendelea kusonga mbele kwa njia zenye nguvu. Idadi hii inayoongezeka ni ushuhuda wa wazi kwamba injili inagusa mioyo na kubadilisha maisha kila mahali.

Katika siku zetu, waongofu hawa wa thamani hawakusanyiki tena katika sehemu moja. Kwa sababu ya imani na kuwekwa wakfu kwa waumini wa Kanisa, rasilimali zinapatikana kusaidia mikusanyiko—kwa ujenzi wa makanisa na mahekalu—kote ulimwenguni. Pamoja na funguo za ukuhani muhimu na rasilimali zinazotolewa, kanuni za kuokoa sasa zinapatikana katika sehemu nyingi za dunia.

Bila kujali tunaishi wapi, waumini wa sasa wanahitaji kukaribisha mamia ya maelfu ya waumini wapya kama tulivyofanya kwa Watakatifu wa Kiingereza na Wales niliowaelezea kutoka historia yetu ya awali. Nilipenda hotuba ya Mzee Gerrit W. Gong katika kipindi hiki ambapo alitufundisha kwamba hakuna mtu anayepaswa kuketi peke yake aidha kihisia au kiroho.

Wajibu wetu mtakatifu ni kuwakubali na kuwakaribisha waumini wapya na wanaorejea. Bwana anapoharakisha kazi Yake, tunapaswa kuwapenda, kuwalea, na kuwatumikia wale wanaokubali injili Yake. Tunaweza kusaidia kujenga watu wa Sayuni, ambapo sisi ni “wa moyo mmoja na nia moja, na [kukaa] katika haki.” Ili kuwa wamoja na Bwana, ni lazima tuwe kitu kimoja mbele za Bwana. Waumini wote bila kujali tarehe ya ubatizo, wanashiriki jukumu la kuwakaribisha wengine.

Ushauri wangu kwa waumini wa Kanisa ni kuwakumbatia kwa mikono yetu hawa wateule wa thamani, ambao wamekubali injili ya Yesu Kristo.

Rais Gordon B. Hinckley alitufundisha kwamba mwongofu mpya anahitaji “rafiki, wajibu, na kulishwa kwa ‘neno jema la Mungu’ (Moroni 6: 4). Sisi ni miongoni mwa marafiki wanaowahakikishia waongofu hawa wapya kuwa ni wa kanisa na si wageni tu. Tunaweza kuwasaidia kuelewa kwamba wao ni wanafunzi wa Yesu Kristo ambao wanaweza kuwahudumia wengine na kukubali miito ya kuhudumu. Vijana walioongoka wanapaswa kuzingatia kutumikia misheni ya muda wote. Wote wanapaswa kuazimia kujitahidi kuishi maisha kama ya Kristo.

Wengi hujiunga na Kanisa kwa kujitolea sana na wanahitaji sana upendo na usaidizi wa Watakatifu wenzao.

Kwa wale ambao ni wapya au wanaorudi kwenye imani, kuna changamoto unaweza kukutana nazo. Kuwa na subira kwako mwenyewe. Wamisionari wamekufundisha fundisho muhimu na kuelezea maagano na ibada za ufalme, ambazo zimewekwa wazi katika maandiko na katika Hubiri Injili Yangu.

Kupokea ibada na maagano na kuishi amri ni muhimu. Zingatia maagano yanayohitajika kwa ajili ya kuinuliwa. Injili inawezesha kuinuliwa, ambako kunahitaji kufanya na kuweka maagano matakatifu na Mungu. Isipokuwa kwa ubatizo, uthibitisho, na utoaji wa Ukuhani wa Melkizedeki kwa wanaume, maagano tunayofanya yanafanywa hekaluni. Kwa wafu, kila moja ya ibada hizi za kuokoa hufanyika tu hekaluni. Ipasavyo, kujitayarisha mwenyewe kwa ajili ya hekalu kunapaswa kuwa lengo la haraka.

Wakati fulani utahisi kutostahili kuhusu kile unachokijua. Maarifa ya injili ni baraka kuu yanayopatikana kidogo kidogo kwa muda mrefu, lakini sio ibada ya kuokoa. Injili sio kipimo cha maarifa. Hata hivyo, kama Rais Nelson alivyoahidi, “Unapojifunza Kitabu cha Mormoni kwa maombi kila siku, utafanya maamuzi bora—kila siku. … Mnapotafakari kile mnachojifunza, madirisha ya mbinguni yatafunguka, na mtapata majibu ya maswali yenu na mwongozo kwa ajili ya maisha yenu.”

Kwa kuongezea, kila mwaka kwa mzunguko mtaala wa Kanisa katika mikutano ya Jumapili hujumuisha Agano la Kale, Agano Jipya, Kitabu cha Mormoni, na Mafundisho na Maagano. Baada ya muda utajisikia kujiamini zaidi kadri maarifa yako ya injili yanavyokua. Kusoma mara kwa mara kwa maandiko kutabariki na kuimarisha maisha yako kwa kuimarisha uongofu wako kwa injili ya Yesu Kristo.

Kujifunza mafundisho safi ya Yesu Kristo ni harakati ya maisha yote, katika kuelewa mafundisho na kuishi maisha kama ya Kristo. Maagano muhimu hutoa mfumo ambao tunaelezea kama njia ya agano. Kanuni hizi zimefundishwa kwa nguvu na Rais Nelson. Waumini wote, hasa wapya na wanaorejea, wangebarikiwa kwa kujifunza na kukubali jumbe zake za kinabii kuhusu maagano na njia ya agano.

Ukiweka lengo la kupokea ipasavyo kila agano linalohitajika kwa ajili ya kuinuliwa, utakuwa kwenye njia inayoongoza kwa ufalme wa selestia. Hekalu na ibada za hekalu zinapaswa kuwa lengo letu. Maagano mengi yanapatikana kwa kila mtu binafsi. Agano moja, ndoa ya milele, inahusisha kuunganisha juhudi zako na mwenzi. Lengo letu linapaswa kuwa kumpata mwenzi huyo wa milele.

Walakini, usivunjika moyo ikiwa ndoa ya milele haiwezekani kwa wakati huu. Manabii wamefundisha kwamba hakuna baraka itakayozuiliwa kutoka kwa waumini waaminifu wanaoshika amri. Nabii mmoja wa Kitabu cha Mormoni, Mfalme Benjamini, alisema hivyo kwa uzuri: “Wale wazishikao amri za Mungu … wamebarikiwa katika mambo yote, … na kama wao [ni] waaminifu hadi mwisho. … wanaweza kuishi pamoja na Mungu katika hali ya furaha isiyo na mwisho”

Utapata, ikiwa bado, kwamba waumini si wakamilifu. Mafundisho yaliyofunuliwa yanaweka wazi kwamba katika ugeni wetu hapa duniani, tutafanya makosa. Tunaishi katika ulimwengu usio kamili na ulioanguka, sio ulimwengu wa selestia. Maisha haya ni wakati wa majaribu, yenye fursa za mara kwa mara za kutubu na kujithibitisha wenyewe.

Sisi sote tunajihisi kuwa hatufai tunapojitahidi kuwa kama Yesu Kristo. Upatanisho Wake huturuhusu kutubu kila siku tunapokosea. Kama vile Nefi, nabii mwingine wa Kitabu cha Mormoni, alivyosema: “[Lazima] tusonge mbele kwa uthabiti katika Kristo, tukiwa na mng’ao mkamilifu wa tumaini, na upendo wa Mungu na wanadamu wote. Kwa hivyo, kama mtasonga mbele, mkila na kusherekea neno la Kristo, na mvumilie hadi mwisho, tazama, hivyo ndivyo asemavyo Baba: Mtapokea uzima wa milele.”

Tunapotafakari changamoto za siku zetu, lazima tukumbuke kwamba Mwokozi, wakati wa huduma Yake duniani, pia aliishi katika nyakati za misukosuko na vurugu. Fokasi Yake haukuwa kwenye changamoto za kisiasa za wakati huo; ilikuwa juu ya ukamilifu wa Watakatifu.

Kumfuata Mwokozi na fundisho Lake na mafundisho Yake haijawahi kuwa rahisi katika ulimwengu ambao daima una msukosuko. Haikuwa rahisi kwa Mwokozi katika ulimwengu wenye hali tete wakati wa kukaa Kwake duniani, na haikuwa rahisi kwa viongozi wetu na waumini wa mapema, na si rahisi kwetu sisi. Kwa bahati nzuri, tuna manabii waliohai ili kutupa mwongozo tunaohitaji hasa kwa ajili ya siku zetu. Rais Dallin H. Oaks ataendeleza urithi huo wenye nguvu kiroho.

Ninashuhudia kwamba fundisho la Kanisa la Yesu Kristo ni la milele na la kweli. Ninatoa ushuhuda wangu wa hakika na kweli kwamba Yesu Kristo anaishi, na kwa sababu ya Upatanisho Wake, tunaweza kuwa na wamoja pamoja naye. Katika jina takatifu la Yesu Kristo, amina.

Muhtasari

  1. Charles Dickens, Hadithi ya Miji Miwili (1859), 1.

  2. Moja ya mada ya Dickens ilikuwa wazo la mabadiliko ya mtu binafsi katika wakati wa machafuko ya kijamii.

  3. Mafundisho na Maagano 45:26.

  4. Ona Gary E. Stevenson, “Heri Wapatanishi,” Liahona, Nov. 2025, 6–9.

  5. Mafundisho na Maagano 1:23.

  6. Ona Mafundisho na Maagano 88:73.

  7. Ona Mafundisho na Maagano 59:23; ona pia Yohana 14:27.

  8. Ona Matendo ya Mitume 2:41.

  9. Ona Mafundisho na Maagano 112. Ufunuo huu ulipokelewa mnamo Julai 23, 1837, siku ambayo injili ilihubiriwa kwa mara ya kwanza nchini Uingereza katika kipindi hiki. Kwa mengi kuhusu misheni hizi, ona James B. Allen, Ronald K. Esplin, na David J. Whittaker, Men With a Mission: The Quorum of the Twelve Apostles in the British Isles, 1837–1841 (1992).

  10. Wengi wa waongofu hawa walitoka kwa madarasa ya kazi. Charles Dickens aliona baadhi yao walipokuwa wakijiandaa kwa safari yao ya kwenda Marekani, kwa meli ya Amazoni. Alikuwa mzuri katika tathmini yake. Aliwaelezea kama, “katika daraja lao, mchumaji na ua la Uingereza” (“The Uncommercial Traveller,” All the Year Round, July 4, 1863, 446). Ona pia 1 Wakorintho 1:26-28.

  11. Ona “Kuwasili kutoka Uingereza, na Mfuko wa Kudumu wa Kuhama,’” Deseret News, Sept. 18, 1852, 90.

  12. Ona Mafundisho na Maagano 76:62, 70; pia ona 1 Corinthians 15:40–42.

  13. Taarifa iliyotolewa na Idara ya Muumini na Kumbukumbu za Takwimu na Umisionari.

  14. Taarifa iliyotolewa na Idara ya Muumini na Kumbukumbu za Takwimu na Umisionari.

  15. Taarifa iliyotolewa na Kumbukumbu za Muumini na Takwimu.

  16. Taarifa iliyotolewa na Idara ya Muumini na Kumbukumbu za Takwimu na Umisionari.

  17. Kufikia miaka ya 1890, viongozi wa Kanisa walianza kuwahimiza washiriki kubaki katika nchi zao za asili badala ya kukusanyika Utah. Vigingi vya kwanza nje ya Intermountain West viliundwa katika miaka ya 1920, na kigingi cha kwanza nje ya Marekani na Kanada kiliundwa nchini New Zealand (ona Brandon S. Plewe, ed., Mapping Mormonism: An Atlas of Latter-day Saint History [2014], 184–85).

  18. Ona Mafundisho na Maagano 110:11–16.

  19. Ona Gerrit W. Gong, “Hakuna Anayeketi Peke Yake,” Liahona, Nov. 2025, 40.

  20. Musa 7:18.

  21. Ona Yohana 5:20-21; 1 Wakorintho 3:-31.

  22. Gordon B. Hinckley, “Converts and Young Men,” Ensign, May 1997, 47).

  23. Ona Yakobo 2:5; pia ona Mathayo 19:29; Warumi 2:11; Waefesos 2:19; Mosia 18:8–9.

  24. Ona Hubiri Injili Yangu: Mwongozo wa Kushiriki Injili ya Yesu Kristo (2023), 17.

  25. Ona Mafundisho na Maagano 14:7.

  26. Russell M. Nelson, “Kitabu cha Mormoni: Maisha Yako Yangekuaje Bila Hicho?,” Liahona, Nov. 2017, 62–63; ona pia Spencer W. Kimball: “Inapoonekana kwamba hakuna sikio la kimungu linalosikiliza, na hakuna sauti takatifu inayozungumza, … kama [sisi] tungezama [wenyewe] katika maandiko umbali ungepunguka na kiroho kurudi” (The Teachings of Spencer W. Kimball (2006), 67.

  27. Ona Yohana 5:39.

  28. Ona, kwa mfano, Russell M. Nelson, “Acheni Mungu Ashinde,” Liahona, Nov. 2020, 92–95; “Nguvu za Msukumo wa Kiroho,” Liahona, Mei 2022, 97–100; “Ushinde Ulimwengu na Upate Pumziko,” Liahona, Nov. 2022, 95–98.

  29. Mosia 2:41.

  30. Ona Alma 34:32.

  31. 2 Nefi 31:20.

  32. Ona Waefeso 4:11–15.

  33. Ona Yohana 17:20–22.