2025
Ili Wote Waweze Kujengwa
Novemba 2025


11:21

Ili Wote Waweze Kujengwa

Tunapofokasi kwa Yesu Kristo, kufundisha mafundisho Yake na kujifunza kwa bidii, tunamkaribisha Roho Mtakatifu kuimarisha imani yetu katika Yesu Kristo na kutusaidia kuwa kama Yeye.

Hadithi inaelezea kuhusu mwanafunzi mdogo wa chuo kikuu ambaye alipambana na darasa lenye changamoto, hivyo alikodisha mkufunzi kumsaidia. Karibu na mwisho wa kozi, profesa alitangaza kwamba wanafunzi wanaweza kuleta kwenye mtihani wa mwisho karatasi moja ambayo wanaweza kuweka chochote wanachotaka. Wanafunzi wengine walijiandaa kwa kutengeneza vidokezo vidogo vya habari kutoka kwa mihadhara na vitabu vya masomo, vinavyosomwa tu kwa lenzi ya kukuza. Lakini kijana mdogo alifika kwenye mtihani wa mwisho akiwa na karatasi tupu na mgeni. Wakati profesa alipomuuliza, kijana mdogo alijibu “Ulisema ningeweza kuleta karatasi moja yenye chochote juu yake.” Kisha akaweka karatasi chini karibu na meza yake na kusema, “Ningependa mkufunzi wangu asimame juu ya karatasi yangu.”

Roho Mtakatifu

Kama waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, tukiwa na baraka ya wenza wa mshiriki wa Uungu, tunaweza kupata msaada wa Mwalimu kamili. Roho Mtakatifu anajua mambo yote, anashuhudia ukweli, na ataleta mambo yote kwenye kumbukumbu [zetu].” Rais Russell M. Nelson alizungumza mara kwa mara kuhusu umuhimu wa kuisikiliza sauti ya Bwana. Alitufundisha jinsi ya kualika ulinzi wa Roho Mtakatifu na alitusihi mara kwa mara sisi tuongeze uwezo wetu wa kiroho wa kupokea ufunuo.

Leo nakualika utafakari jukumu la Roho Mtakatifu, hasa kuhusiana na kujifunza na kufundisha injili nyumbani na kanisani. Roho Mtakatatifu hutolewa kwa sala ya imani na tunapojitahidi kuishi kwa kustahili kipawa hiki cha thamani. Kitabu cha Kiada cha Kanisa Kufundisha katika Njia ya Mwokozi kinabainisha kanuni za ziada ambazo Bwana amezianzisha ambazo zitasaidia kualika ushawishi wa Roho Mtakatifu.

Alika Kujifunza kwa Bidii

Moja ya kanuni hizi ni kualika kujifunza kwa bidii. Hapo zamani, tunaweza kuwa tulidhani kwamba kufundisha ni fursa kwa mzazi au mwalimu kumkaribisha Roho katika maandalizi yao wenyewe na kisha kushiriki kile walichojifunza na watoto au darasa, ambao jukumu lao lilikuwa kusikiliza. Lakini bora zaidi ni wakati sisi, kama wanafunzi, pia kujiandaa na pale walimu wanapotengeneza uzoefu wa kujifunza ambao unakidhi ufunuo binafsi moja kwa moja kwenye mioyo na akili zetu. Kisha, tunapopata fursa za kushiriki kile tunachojifunza kupitia masomo yetu na kutoka kwa Roho Mtakatifu tunaweza kusaidiana kuelekezwa na kujengwa. Tunapokuwa tukitumia kanuni za injili, Roho tena atashuhudia ukweli wake.

Fursa za kushiriki

Kama katika vitu vyote, Yesu Kristo ni mfano sahihi. Amemwalika kila mmoja wetu kuwa wanafunzi mwenye bidii na kushughulikia shuhuda zetu wenyewe. Aliwaalika wanafunzi Wake kujiandaa kujifunza, kushiriki yale waliyokuwa wanajifunza, na kutenda kwa imani. Aliomba kwa ajili yao, aliona uwezekano wao wa kiroho, aliwasikiliza, na kuwasaidia kujua kuwa walipendwa na kuhitajika.

Kama walimu, tunaweza kuzingatia zaidi maendeleo ya mwanafunzi, kukidhi mahitaji yao, na kuwasaidia kukuza tabia za kiroho za ufuasi wa maisha yote. Kama wanafunzi, tunapofanya kazi kwa uamuzi wetu katika mchakato wa kujifunza, tunamwonyesha Roho Mtakatifu kutaka kwetu kufundishwa Naye.

Nina shukuru kwa mwalimu ambaye alinialika niwe mwanafunzi bora. Nilipokuwa naanza chuo kikuu, nilifikiri vibaya kuhusu shule kama kitu cha kustahimili ili niweze kucheza michezo. Siku moja, baada ya kusoma insha niliyoandika, profesa wangu alinambia alidhani mimi ni mfikiriaji mzuri wa kiuchambuzi. Sikuwa na hata ufahamu wa maana yake. Alisema kwamba kwa juhudi zaidi zenye mtazamo uliozingatiwa, naweza kuwa mwanafunzi mzuri. Wazo hilo lilikuwa halijawahi kupita akilini mwangu. Hamu yake, himizo na mwaliko vilibadilisha mkondo wa elimu yangu na kuja kunibariki sana katika maisha yangu.

Fundisha Mafundisho

Kanuni nyingine sambamba na kumwalika Roho Mtakatifu ni kufundisha mafundisho ya kweli. Hii ina maana kwamba mafunzo yetu ya injili na maelekezo vina msingi katika neno la Mungu na kwamba hatufanyi mambo kuwa makubwa au kubashiri kuhusu kile ambacho Bwana hajadhihirisha. Badala yake, tunazingatia kanuni muhimu na za milele za injili, ambazo zinamwezesha Roho kutoa ushuhuda wa ukweli. Tena, tunafuata mfano wa Mwokozi. Alisema, “Mafunzo yangu si yangu mimi, ila ni yake yeye aliyenipeleka.”

Mafundisho ya kweli yanapatikana katika maandiko na katika mafundisho ya manabii wa siku hizi. Mwaliko wa Bwana wa kujifunza maandiko binafsi na kama familia na kuhudhuria kanisani kila wiki kujifunza injili Yake unatoa mfumo mzuri wa kujifunza mafundisho Yake na kuisikia sauti Yake. Tunapekua maandiko ili kuelewa simulizi, kanuni wanazofundisha na matumizi ya kweli hizi katika maisha yetu. Ni baraka kubwa kiasi gani kuwa na maandiko mikononi mwetu. Fikiria Adamu na Hawa, Abinadi, au hata Mwalimu Mkuu Yesu Kristo wakitembelea nyumba zetu au madarasa yetu ili kutufundisha. Wanaweza kama tunasherehekea neno la Mungu. Kwa juhudi endelevu, tunaweza kujifunza kuelewa na kupenda maandiko na kuamini kwamba yana majibu ya maswali ya nafsi.

Kulikuwa na wakati kabla ya kuoana kwetu ambapo mke wangu Kristi, alikuwa anasumbuka kuhisi upendo wa Baba wa Mbinguni na kuelewa mpango Wake kwa ajili yake. Alipokuwa akiomba mwongozo, wazo lilikuja kwamba anapaswa kuhudhuria chuo (institute), hivyo alijiandikisha katika darasa la Agano Jipya. Jinsi mwalimu wake wa darasa hilo alivyofundisha kutoka kwenye maandiko, hata jinsi alivyoshika maandiko hayo, ilionyesha jinsi alivyolipenda neno la Mungu. Alipohudhuria, Roho Mtakatifu alimnong’oneza kwamba kulikuwa na kitu katika maandiko ambacho alikihitaji. Upendo wa mwalimu wake kwa maandiko na mwongozo wa Roho Mtakatifu vilimpa tamanio la kuanza kujifunza kwa makini neno la Mungu—ambalo lilikuwa safari ya maisha ya uongofu wa kina na huduma iliyowekwa wakfu.

Fokasi kwa Yesu Kristo

Hatimaye, kama Kufundisha katika Njia ya Mwokozi inavyopendekeza, kufundisha na kujifunza kwetu lazima kufokasi kwa Yesu Kristo. Tunaweza kuzungumza zaidi mara kwa mara na kwa heshima zaidi kuhusu Yeye na kutafuta nafasi zaidi za kutoa ushuhuda, shukrani na upendo Kwake. Iwe katika mazingira yoyote, tunapomkumbuka, tunaweza kuwa na “Roho wake awe pamoja [nasi]”

Njia moja ya kumweka Yesu Kristo katikati ya mafundisho yetu ni kuonyesha kwamba Yeye ndiye mfano mkamilifu, halisi na dhihirisho la kanuni zote za injili. Hata pale ambapo Hajatajwa moja kwa moja katika simulizi ya maandiko, bado tunaweza kumuona kama kielelezo cha kanuni inayofundishwa. Tunaweza kuuliza kwa urahisi, “Je, unaweza kukumbuka wakati ambao Yesu Kristo alikuwa mfano wa kanuni hii?”

Tunaweza pia kufokasi Kwake kwa kujifunza majina, majukumu, na sifa Zake, kujifunza si tu kuhusu kile alichofanya bali kuelewa vyema kuhusu Yeye ni nani. Kwa mfano, tunapojifunza kanuni ya toba, ni muhimu kuelewa jinsi ya kutubu. Lakini pia ni muhimu kukumbuka kile Yesu Kristo alichokifanya kuwezesha toba na kuelewa kile toba inachotufundisha kumhusu Yeye, kuhusu asili Yake ya kweli na tabia Zake. Fursa yetu ya kutubu inasema nini kuhusu upendo Wake, uvumilivu na rehema, imani Yake katika uwezo wetu wa kimungu, utayari Wake wa kulipia dhambi zetu na furaha anayoipata katika kusamehe? Na kuelewa majina Yake—kama vile Mwanakondoo wa Mungu, Mkombozi na Tabibu—kunatusaidia kuona kwamba toba ni mwaliko Wake wa kusafisha, kubadilisha na kutuponya. Kufokasia yale ambayo ameyafanya kwetu na yale yasemwayo kuhusu Yeye yanaweza kutusaidia kuwa na “imani iongozayo kwenye toba.”

Wakati fulani, tunaweza tusione kwa haraka tabia za Mwokozi zilizoelezwa kwenye hadithi za maandiko. Kwa mfano, tunaposoma kuhusu Nefi akijenga mashua, tunaweza kumfokasia zaidi Nefi. Lakini kumfokasia Mwokozi kunaweza kutusaidia kuona kwamba rekodi hii haikuhifadhiwa kutufundisha kuhusu ukuu wa Nefi bali kutuonyesha ukuu wa Mungu—kwamba Anatupa nguvu za kuzishika amri Zake na kutuokoa katika nyakati za shida.

Tunaweza pia kufokasia jukumu kuu la Yesu Kristo katika mpango mkamilifu wa furaha wa Baba wa Mbinguni. Inaweza kubadili mwelekeo wa maisha yetu kuona hali zetu kupitia lenzi ya mpango wa milele wa Mungu badala ya kuona mpango huo kupitia lenzi ya hali zetu za muda. Injili si orodha ya mahitaji; ni habari njema kwamba Yesu Kristo alishinda dhambi na kifo. Ni kwa kufikia neema Yake ya ajabu kwa kutunza maagano yetu na Mungu ndipo tunaweza kuishi kwa furaha sasa na kujiandaa kwa maisha pamoja na Baba yetu Mbinguni katika umilele. Tunapojifunza kumuona Baba wa Mbinguni na Mwokozi katika maandiko, tutakuja kuwaelewa vizuri zaidi na tutayaona mapenzi Yao na ushawishi wao mara nyingi na kwa nguvu zaidi katika maisha yetu.

Daima nitamkumbuka Roho niliyemhisi nikiwa kijana wakati mwalimu wetu alipofundisha kuhusu siku za mwisho za maisha ya Mwokozi. Alitusaidia kuona umuhimu wa matukio katika chumba cha juu, Gethsemane, Golgotha na kaburi lililokuwa tupu. Alishiriki shukurani zake za dhati kwa Mwokozi na tamanio lake kubwa la kumfuata. Mafundisho yake yalikuwa mwaliko kwa Roho Mtakatifu kushuhudia kuhusu Yesu Kristo. Roho niliyoihisi katika darasa hilo aliongeza kina cha imani yangu na kuongeza upendo na shukrani zangu kwa Mwokozi. Ushawishi wa mwalimu huyo umebaki nami maisha yangu yote. Kama ilivyosemwa kuhusu mwalimu mwingine, “Tungeweza kupasha mikono yetu moto kwa imani yake.

Hitimisho

Katika mikutano nyumbani na Kanisani, tunapofokasi kwa Yesu Kristo, kufundisha mafundisho Yake na kujifunza kwa bidii, tunamkaribisha Roho Mtakatifu kuimarisha imani yetu katika Yesu Kristo na kutusaidia kuwa kama Yeye, ambalo ndilo lengo la kufundisha na kujifunza injili.

Mchoro wa kufundishia

Nina shukrani kwa walimu katika maisha yangu, kutoka kwa wazazi wema na viongozi wa eneo husika na walimu hadi kwa wanaume na wanawake ambao wameitwa kufundisha na kushuhudia kutoka kwenye mimbari hii, wanaotusaidia kumjua na kumfuata Yesu Kristo. Na ninashukuru kwa Roho Mtakatifu, mwalimu mzuri. Ni kupitia Roho Mtakatifu ambapo najua kwamba Baba wa Mbinguni anatupenda na anao mpango mkamilifu kwa ajili yetu; kwamba Yesu ni Kristo, Mwokozi na Mkombozi wa dunia, na kwamba injili na Kanisa Lake vimerejeshwa. Nashuhudia kwa shukrani kuhusu mambo haya katika jina la Yesu Kristo, amina.