2025
Joseph Anafariki kwa ajili ya Injili
Novemba 2025 Rafiki


“Joseph Anafariki kwa ajili ya Injili,” Rafiki, Novemba 2025, 26–28.

Hadithi za Maandiko

Joseph Anafariki kwa ajili ya Injili

Watu wa mji wenye hasira wakisoma gazeti

Watu wengi walikasirishwa na Joseph Smith na Kanisa. Hawakupenda kile Jpseph alichokuwa akifundisha. Baadhi ya watu hata walitaka kumuua.

Joseph Smith akiikumbatia familia yake

Joseph alipaswa kwenda katika mji wa Carthage ili hakimu aweze kuamua kama alikuwa amevunja sheria. Joseph alimbariki Emma na watoto wake, akawabusu akiwaaga, na akaondoka kwenda Carthage.

Joseph na Hyrum wakiendesha farasi na kuangalia nyuma kwenye Hekalu la Nauvoo lililokuwa halijakamilika

Hyrum, kaka yake Joseph na marafiki wengine walikwenda pamoja naye. Walipokuwa wakiondoka, Joseph alitazama nyuma huko Nauvoo. “Hapa ni mahali pa kupendeza zaidi na watu bora chini ya mbingu,” alisema.

Joseph katika Jela ya Carthage akizungumza na walinzi, wakati Hyrum akisoma maandiko

Katika Carthage wanaume hawa waliwekwa jela. Hyrum aliwasomea kutoka kwenye Kitabu cha Mormoni. Joseph aliwaambia walinzi kwamba Kitabu cha Mormon ni cha kweli.

Wanaume wenye bunduki wakijaribu kuingia chumbani wakati Joseph na marafiki zake wakishikilia mlango ukiwa umefungwa

Baadaye siku hiyo, wanaume wenye hasira wakiwa na bunduki walikimbia haraka na kuingia jela. Walianza kupiga risasi ndani ya chumba ambamo Joseph na marafiki zake walikuwemo. Hyrum na Joseph waliuawa.

Watakatifu wa mwanzo wakifarijiana na Hekalu la Nauvoo likiwa nyuma yao juu ya mlima

Watakatifu walikuwa na huzuni sana walipogundua kwamba Joseph na Hyrum walikuwa wamefariki. Lakini walijua kwamba Kanisa lingeendelea kukua na kuwabariki watoto wa Mungu ulimwenguni kote.