“Maneno Yangu ya Injili,” Rafiki, Novemba 2025, 10.
Maneno Yangu ya Injili
Tafuta maneno haya na virai katika toleo hili la jarida la Rafiki!
Zaka
Kulipa zaka ni kurudisha kwa Baba wa Mbinguni kwa kuchangia sehemu moja ya kumi (asilimia 10) ya pesa tunazopata kwa Kanisa Lake. Zaka husaidia kujenga mahekalu na makanisa na kusaidia kazi ya Kanisa. Tunapolipa zaka, Baba wa Mbinguni hutubariki katika njia nyingi!
Mababu
Mababu zetu ni watu katika familia yetu ambao waliishi muda mrefu uliopita, kama babu na bibi wakuu wetu. Mababu ni sehemu muhimu ya historia ya familia yetu. Tunaweza kujifunza kuwahusu wao, kuwakumbuka, na kufanya kazi ya hekaluni kwa niaba yao ili tuweze kuwa pamoja nao milele.
Farahisisha
Kufarahisisha ni njia tunayoweza kuwasaidia wengine kuwapata mababu wao! Tunaandika majina kutoka kwenye kumbukumbu za zamani za karatasi kwenye kompyuta ili watu waweze kuwatafuta wanafamilia wao na kupata kumbukumbu kuhusu maisha yao. Hii inasaidia kwenye historia ya familia na kazi ya hekalu ili watu wengi zaidi waweze kuunganishwa pamoja milele. Hata watoto wanaweza kusaidia kwenye kufarahisisha!
Kifo cha kishahidi
Kifo cha kishahidi hutokea wakati mtu anapokufa kwa ajili ya kitu wanachoamini. Joseph Smith na kaka yake Hyrum walikuwa wafia dini kwa sababu waliuawa kwa ajili ya walichoamini, walichoishi, na kufundisha injili ya urejesho ya Yesu Kristo.
Vielelezo na Madison Baker