Kikao cha Jumamosi Mchana
Hakuna Anayeketi Peke Yake
Dondoo
Afrika Kusini
Estonia
Katika mfano wa Msamaria mwema, Yesu anatualika tuje kwa kila mmoja wetu pamoja na Kwake katika nyumba Yake ya wageni—Kanisa Lake. …
Roho ya “chumba katika nyumba ya wageni” inajumuisha “hakuna anayeketi peke yake.” Unapokuja kanisani, ukiona mtu yuko peke yake, tafadhali msalimie na kuketi naye? …
“Hakuna anayeketi peke yake” pia inamaanisha hakuna anayeketi peke yake kihisia au kiroho. Wakati fulani nilienda na baba aliyevunjika moyo kumtembelea mwanawe. Miaka mingi kabla, mwana huyo alifurahi kuwa shemasi mpya. Kwa hafla hiyo, familia yake ilimnunulia jozi yake ya kwanza ya viatu vipya.
Lakini kanisani, mashemasi walimcheka yeye na viatu vyake. Viatu vyake vilikuwa vipya, lakini si vya kisasa. Kwa aibu na maumivu, shemasi huyo mdogo alisema kamwe hangeenda tena kanisani. Moyo wangu bado umevunjika kwa ajili yake na familia yake. …
Katika Kanisa Lake lililorejeshwa, sisi sote ni bora wakati hakuna anayeketi peke yake. Tusikubaliane tu au tuvumilie. Tuwakaribishe kwa dhati, tuwatambue, tuwatumikie, tuwapende. …
Leo wengi huhisi upweke na kutengwa. …
Kuna sababu nyingi ambazo tunaweza kuhisi kwamba hatufai kuwa kanisani—kwamba, tukizungumza kwa njia ya kitamathali, tunaketi peke yetu. …
Mosia 18:21 inatualika kufuma mioyo yetu pamoja katika upendo. Ninakualikeni sote tupunguze wasiwasi, tusihukumu sana, tusitake mengi kutoka kwa wengine—na, inapohitajika, tusiwe wagumu juu yetu wenyewe.
Agano la kuwa sehemu ya linaongezeka kina tunapokuja kwa kila mmoja wetu na kwa Bwana katika nyumba Yake ya wageni. Bwana hutubariki sisi sote pale ambapo hakuna anayeketi peke yake.