Kikao cha Jumapili Asubuhi
Nimethibitishwa na Kuimarishwa katika Kristo
Dondoo
Peru
Miaka mingi iliyopita, nilitafuta kujifunza fizikia na hisabati katika miaka yangu ya chuo kikuu. Nilihisi kuzidiwa. … Nilianza kufikiria kuacha, na kufanya kitu kilicho rahisi zaidi.
Nilihisi kuwa dhaifu. Niliposali, nilihisi hakikisho tulivu la Bwana. Nilimhisi Yeye akiiambia akili yangu, “ninakuthibitisha wewe, lakini pia niko pamoja nawe.” …
Nilikuja kujua kwamba mapambano yangu katika fizikia kwa kweli yalikuwa ni zawadi kutoka kwa Bwana. Alikuwa akinifundisha kwamba kwa msaada Wake, ningeweza kufanya mambo ambayo yalionekana kuwa hayawezekani ikiwa nitakuwa na imani kwamba Yeye angekuwa hapo ili kunisaidia. Kupitia zawadi hii, Bwana alikuwa akifanya kazi ili kunithibitisha na kuniimarisha.
… Ili kukithibitisha kipande cha chuma ni kukiweka chini ya mkazo. … Chuma hakifanywi kuwa dhaifu kwa sababu ya kuthibitishwa. Kwa kweli, kinakuja kuwa kitu fulani ambacho kinaweza kuaminiwa, kitu chenye nguvu vya kutosha kuhimili mzigo mkubwa zaidi. …
Tunapoendelea kuwa na imani katika Yesu Kristo—hata wakati mambo yanapoonekana hayawezekani kwetu kwa wakati huo—tunakuwa imara zaidi kiroho. …
Kwa sababu ya Upatanisho Wake Mtukufu, Yesu Kristo anaweza kutuimarisha sisi katika nyakati zetu za majaribu. …
… Kunawezekana kukaja kimya kimya, kupitia majaribu ya maisha ya familia. Kunaweza kuja kupitia ugonjwa au kukatishwa tamaa au huzuni au upweke.
Ninatoa ushuhuda kwamba nyakati hizi sio ushahidi kwamba Bwana amekutelekeza. Badala yake, ni ushahidi kwamba anakupenda kiasi cha kutosha kukusafisha na kukuimarisha. Anakufanya wewe uwe imara vya kutosha kuweza kubeba uzito wa uzima wa milele.