Kwenye Hoja
Kwa nini maandiko yanazungumza kuhusu Uumbaji wa dunia?
Uumbaji, na Annie Henrie Nader
Maandiko yanazungumza kuhusu Uumbaji ili kutufundisha kusudi lililo nyuma yake badala ya michakato inayohusiana na uumbaji huo.
Wakati Musa alipomwomba Bwana “kumwambia [yeye] kuhusiana na dunia hii … na pia mbingu,” Bwana alisema, “Hii ni kazi yangu na utukufu wangu—kuleta kutokufa na uzima wa milele wa mwanadamu” (Musa 1:36, 39).
Wakati Bwana alipomfundisha Ibrahimu kuhusu Uumbaji, Yeye alimwonyesha Baraza la Mbinguni, ambapo watoto wa kiroho wa Mungu walikuwa wamekusanyika. Ibrahimu alimwona Yesu Kristo kabla ya kuzaliwa akielezea:
“Sisi tutakwenda chini, kwani kuna nafasi huko, nasi tutachukua vifaa hivi, nasi tutaifanya dunia, mahali ambapo hawa watapata kukaa;
“Nasi tutawajaribu kwa njia hii, ili kuona kama wao watafanya mambo yote yale ambayo Bwana Mungu wao atawaamuru;
“… Na wale watakaoitunza hali yao ya pili watapata kuongezewa utukufu juu ya vichwa vyao kwa milele na milele” (Ibrahimu 3:24–26).
Uumbaji mkubwa na mtukufu wa Mungu, ikijumuisha dunia hii, ni sehemu ya mpango Wake wa kutusaidia sisi, watoto Wake, kupokea wokovu na kuinuliwa.