Kikao cha Jumapili Asubuhi
Nyakati za Kufanywa Upya kwa Vitu Vyote
Dondoo
Uanzishwaji rasmi wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ulikuwa umefikia kilele cha mlolongo wa matukio ya kimiujiza. …
Kutokea huku kwa Baba na Mwana kwa Joseph Smith, tafsiri na kuibuka kwa Kitabu cha Mormoni na urejesho wa mamlaka na funguo za ukuhani vilikuwa vitu muhimu vilivyopasa kutangulia kuanzishwa kwa Kanisa la Bwana liliorejeshwa miaka 195 iliyopita siku kama ya leo.
… Mwaka mmoja baada ya kuanzishwa kwa Kanisa, Bwana alielekeza Joseph Smith kwamba funguo za ufalme wa Mungu zilikuwa tena “zimekabidhiwa kwa mwanadamu duniani” na “injili [ya Yesu Kristo] ingeenea hata miisho ya dunia, kama vile jiwe lililochongwa mlimani bila mikono.”
Ninashuhudia: Bwana anatimiza ahadi Yake. …
… Kama sehemu ya urejesho uliotabiriwa wa mambo yote katika siku za mwisho, manabii na mitume wa kale binafsi walitunukia mamlaka ya ukuhani juu Joseph Smith na kukabidhi funguo za ukuhani kwake. …
Kazi ya Bwana katika siku za mwisho “ni jukumu ambalo limewavutia watu wa Mungu kwenye kila enzi; ni dhima ambayo kwayo manabii, makuhani na wafalme wamestaajabia; wametazamia kwa matamanio ya shangwe kwenye siku ambayo sisi tunaishi; na wakiwa na shauku ya kimbunga na matarajio ya furaha wameimba na kuandika na kutoa unabii wa hii siku yetu.”…
Habari njema na tukufu zaidi ya mtu yeyote ulimwenguni anaweza kupokea ni kwamba Bwana Yesu Kristo amerejesha injili Yake na Kanisa Lake katika siku za mwisho.
Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ni Kanisa la Kristo la Agano Jipya limerejeshwa.