Kikao cha Jumapili Asubuhi
Zawadi Kuu za Milele: Upatanisho wa Yesu Kristo, Ufufuko, Urejesho
Dondoo
Miaka mingi iliyopita, darasa letu la injili la mapema asubuhi lilikuwa la kukariri mistari ya Biblia. Kwa kweli mimi nilivutiwa na vifungu vya maneno vifupi. Hii ilijumuisha Yohana 11:35—aya fupi zaidi katika maandiko, ni maneno mawili tu—“Yesu alilia.”
Kwangu mimi sasa, kwamba Yesu analia kwa huzuni na shangwe inashuhudia juu ya uhalisia wa kimiujiza: Mwana mtakatifu wa Mungu alikuja kimwili duniani na akajifunza kulingana na mwili jinsi gani daima anaweza kuwa nasi na kutubariki.
Tunalipolia kwa huzuni au shangwe, Yesu Kristo anaelewa kikamilifu kabisa. Yeye anaweza kuwa yupo katika nyakati ambazo tunahitaji zaidi zawadi kuu za milele: Upatanisho wa Yesu Kristo, Ufufuko, urejesho. …
Pasaka katika Yesu Kristo hutufanya sisi tuhisi idhinisho la Mungu. Ulimwengu huu unatuambia kwamba sisi ni warefu sana, wafupi sana, wapana sana, wembamba sana, wajanja sana—tusio na akili sana, warembo, au wa kutosha kiroho. Kupitia mabadiliko ya kiroho katika Kristo sisi tunaweza kuepuka ukamilifu wa kulemaza. …
Mpango wa Mungu juu ya maadili na haki ya kujiamulia duniani vinaturuhusu kujifunza kwa uzoefu wetu sisi wenyewe. … Katika upendo, Yesu Kristo alijishusha chini na kupanda juu ya vitu vyote. Yeye anafurahia katika uwezo wetu wa kiungu wa ubunifu na furaha, ukarimu pasipo matumaini ya thawabu, imani katika toba na msamaha. Na analia kwa huzuni kwa wingi wa mateso yetu ya mwanadamu, ukatili, ukosefu wa haki—mara nyingi huletwa na uchaguzi wa mwanadamu—kama vile mbingu na Mungu wa mbinguni pamoja nao. …
Hii ni Pasaka katika Yesu Kristo: Yeye anajibu matamanio ya mioyo yetu na maswali ya nafsi zetu. Yeye anafuta machozi yetu, isipokuwa machozi yetu ya shangwe.