2025
“Hivyo Watu Wote Watatambua Ya Kuwa Ninyi Mmekuwa Wanafunzi Wangu”
Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana Mei 2025


Kikao cha Jumamosi Mchana

“Hivyo Watu Wote Watatambua Ya Kuwa Ninyi Mmekuwa Wanafunzi Wangu”

Dondoo

alt text

Pakua PDF

“Mpendane,” Yesu alisema. “Hivyo Watu Wote Watatambua Ya Kuwa Ninyi Mmekuwa Wanafunzi Wangu.” Mara nyingi sana, ushuhuda wa kwanza wa mtu juu ya Yesu Kristo huja wakati anapohisi upendo miongoni mwa wanafunzi wa Yesu Kristo. …

Mtu yeyote anayetafuta imani kuu zaidi katika Kristo au muunganiko wa karibu zaidi na Baba wa Mbinguni anapaswa kuhisi yuko nyumbani katika Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. …

Kwa hivyo, tunaposhikilia viwango vya juu vya Bwana, tuwe na subira pia na sisi kwa sisi. …

Na kuwa wa moyo mmoja, tunapaswa kutafuta mioyo safi, na hilo linahitaji badiliko kuu la moyo.

Lakini hiyo haimaanishi kubadilisha moyo wangu ili uendane na wako. Wala haimaanishi kubadilisha moyo wako ili kuendana na wangu. Inamaanisha sisi sote tunabadilisha mioyo yetu ili kuendana na Mwokozi. …

Na ikiwa unaona kama hapakufai kabisa, tafadhali fahamu kuwa hauko peke yako. …

… Sisi tu wamoja, si kwa sababu ya mahali tulipokuwa bali pale tunapojitahidi kwenda, si kwa sababu ya sisi ni nani bali vile tunavyotafuta kuwa.

Hivyo ndivyo Kanisa la kweli la Kristo lilivyo. …

Na vipi kama wewe ni tofauti na watu walio karibu nawe? Hiyo haikufanyi kuwa mtu asiyefaa—inakufanya wewe uwe sehemu inayohitajika ya mwili wa Kristo. …

Hiyo haimaanishi kuwa kazi yako ni kubadilisha kila mtu kuwa kama wewe ulivyo. Lakini inamaanisha kwamba una jambo muhimu la kuchangia—na kwamba una jambo muhimu la kujifunza!