2025
“Songeni Karibu Nami”
Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana Mei 2025


Kikao cha Jumamosi Asubuhi

“Songeni Karibu Nami”

Dondoo

alt text

Pakua PDF

Kuna nyakati tunahisi kuwa karibu na Mwokozi Yesu Kristo. Na bado, wakati mwingine wakati wa majaribu yetu ya duniani, tunahisi umbali fulani kutoka Kwake na tunatamani hakikisho kwamba Yeye anajua kile kilicho katika mioyo yetu na anatupenda kama watu binafsi. …

Yesu Kristo anampenda kila mmoja wetu. Yeye hutupa fursa ya kumkaribia Yeye zaidi. Kama vile rafiki mwenye upendo, utafanya katika njia sawa na hiyo, kwa kuwasiliana kupitia sala na Baba wa Mbinguni katika jina la Yesu Kristo, kusikiliza mwongozo wa thamani kutoka kwa Roho Mtakatifu na kuwatumikia wengine kwa ajili Mwokozi kwa furaha. …

Kama vile kwa wanafunzi wake wapendwa, kila mtoto wa Baba wa Mbinguni ambaye amechagua kuingia kupitia lango la ubatizo yuko kwenye agano la kuwa shahidi wa Mwokozi na kwa maisha yote kuwatunza wale wenye uhitaji. …

Mnapokuwa wakweli kwenye ahadi hizi, mtagundua kwamba Bwana hutimiza ahadi Zake za kuwa nanyi kwenye huduma yenu, akifanya mizigo yenu kuwa miepesi. Mtakuja kumjua Mwokozi, na baada ya muda mtakuwa kama Yeye na “kukamilishwa kupitia Yeye.” Kwa kuwasaidia wengine kwa ajili ya Mwokozi, mtagundua kwamba mnasonga karibu Naye. …

Mnapofunga vidonda vya wale wenye uhitaji, nguvu ya Bwana itawasaidia. Mikono Yake itanyooshwa na yako ili kuwasaidia na kuwabariki watoto wa Baba yetu wa Mbinguni.

Kila mtumishi wa agano wa Yesu Kristo atapokea mwongozo Wake kutoka kwa Roho pale wanapobariki na kuwatumikia wengine kwa niaba Yake. Kisha wao watahisi upendo wa Mwokozi na kupata shangwe ya kusonga karibu Yake.