Rafiki
Musa Nabii
Machi 2026


“Musa Nabii,” Rafiki, Machi 2026, 46–48.

Njoo, Unifuate

Musa Nabii

Musa katika mavazi ya Kimisri akimtazama Mmisri akimtendea vibaya mtumwa Muisraeli

Musa alikuwa Muisraeli, lakini alilelewa na binti wa Farao huko Misri. Musa alihuzunika kwamba Wamisri walikuwa wakatili kwa Waisraeli na kuwafanya kuwa watumwa wao.

Musa akiwa ameweka mkono wake kumzunguka mtumwa Muisraeli, akimsaidia

Siku moja Musa alimwona Mmisri akimpiga Muisraeli. Musa alimtetea Muisraeli.

Musa akiwa peke yake nyikani

Farao alipogundua, alitaka kumuua Musa, lakini Musa alikimbia kutoka Misri.

Musa akiwa pamoja na mke wake na watoto.

Musa alienda mahali palipoitwa Midiani, ambapo alikutana na mwanamke aliyeitwa Sipora. Walioana na kupata watoto.

Musa anamwona Bwana katika kichaka kinachowaka moto

Wakati akiishi huko Midiani, Musa aliona kichaka kilichokuwa kikiwaka moto, lakini moto ule haukuunguza kile kichaka. Bwana alitokea katika moto ule na kuzungumza na Musa.

Bwana akizungumza na Musa

Bwana alisema alijua Waisraeli walikuwa wakiteseka Misri. Alimwamuru Musa kurudi Misri na kumwambia Farao kuwaachia Waisraeli waende zao. Bwana alisema angemsaidia Musa kuwaweka huru Waisraeli na kuwaongoza kwenye nchi ya ahadi.