“Musa Nabii,” Rafiki, Machi 2026, 46–48.
Njoo, Unifuate
Musa Nabii
Musa alikuwa Muisraeli, lakini alilelewa na binti wa Farao huko Misri. Musa alihuzunika kwamba Wamisri walikuwa wakatili kwa Waisraeli na kuwafanya kuwa watumwa wao.
Siku moja Musa alimwona Mmisri akimpiga Muisraeli. Musa alimtetea Muisraeli.
Farao alipogundua, alitaka kumuua Musa, lakini Musa alikimbia kutoka Misri.
Musa alienda mahali palipoitwa Midiani, ambapo alikutana na mwanamke aliyeitwa Sipora. Walioana na kupata watoto.
Wakati akiishi huko Midiani, Musa aliona kichaka kilichokuwa kikiwaka moto, lakini moto ule haukuunguza kile kichaka. Bwana alitokea katika moto ule na kuzungumza na Musa.
Bwana alisema alijua Waisraeli walikuwa wakiteseka Misri. Alimwamuru Musa kurudi Misri na kumwambia Farao kuwaachia Waisraeli waende zao. Bwana alisema angemsaidia Musa kuwaweka huru Waisraeli na kuwaongoza kwenye nchi ya ahadi.