“Safari ya Wiki Takatifu Yote,” Rafiki, Machi 2026, 14–15.
Safari ya Wiki Takatifu Yote
Yerusalemu
Siku ya Jumapili ya Matawi, watu walimpokea Yesu Kristo wakati alipokuja Yerusalemu. Walipiga makelele ya “Hosana” ili kusherehekea. Hosana ni neno la Kiebrania likimaanisha “tafadhali tuokoe.”
Katika usiku wa Karamu ya Mwisho, Yesu aliosha miguu ya wanafunzi Wake. Aliweka mfano wa huduma ya unyenyekevu ili sisi tuufuate.
Bustani ya Gethsemane
Katika Bustani ya Gethsemane, Yesu Kristo alisali na kuhisi maumivu na matatizo ya kila mtu. Aliteseka kwa ajili ya dhambi zetu.
Kaburi
Yusufu wa Arimathaya aliomba kama angeweza kuushughulikia mwili wa Yesu Kristo baada ya kufa Kwake. Yusufu alitoa kaburi lake mwenyewe jipya kwa ajili ya Yesu kuwa na mahali pazuri pa kupumzika.
Mariamu Magdelena alikuwa mtu wa kwanza kumwona Mwokozi baada ya Ufufuko Wake. Alikimbia kuwaambia Mitume habari njema!
Mabara ya Amerika
Baada ya kifo Chake, Yesu Kristo aliwatembelea “kondoo Wake wengine” kote ulimwenguni. Sehemu moja aliyoitembelea ilikuwa ni Mabara ya Amerika. Waligusa majeraha katika mikono na miguu Yake na walijua kwamba Yule Alikuwa Mwokozi aliyefufuka.
Kielelezo na Dave Klüg Kinaweza kunakiliwa kwa matumizi ya Kanisa pekee.