“Kwa Maana Jinsi Hii Mungu Aliupenda Ulimwengu,” Rafiki, Machi. 2026, 2–3.
Kutoka kwa Urais wa Watoto
Kwa Maana Jinsi Hii Mungu Aliupenda Ulimwengu
Baba wa Mbinguni anatupenda sisi sote sana kiasi kwamba alimtuma Mwanawe, Yesu Kristo, kutusaidia kurudi Kwake.
Yesu alijua kungekuwa na nyakati katika maisha yetu ambapo tungehisi huzuni, maumivu, na upweke. Tungefanya makosa na hata kuwa na woga wakati mwingine. Katika Bustani ya Gethsemane, Yesu Kristo alichagua kuhisi vitu hivyo vyote ili aweze kuelewa na kutusaidia kikamilifu. Pia alilipia dhambi zetu ili tuweze kutubu. (Ona Alma 7:11–13.)
Yesu pia alijua kwamba wakati utakapofika, sote tungekufa. Kifo ni sehemu ya asili na ya kawaida ya maisha. Lakini Mungu hakutaka kifo kiwe mwisho wa hadithi yetu. Kwa sababu Yesu Kristo alitoa uhai Wake na kufufuka, sisi sote tutaishi tena. Hiyo ndiyo sababu Yeye alichagua kufa kwa ajili yetu.
Tunaita kile Mwokozi alikifanya Upatanisho wa Yesu Kristo. Zawadi hii takatifu ilifanyika kwa ajili yetu kwa upendo. Kumbuka, Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtuma Mwanawe, Yesu Kristo (ona Yohana 3:16). Na Yesu alitupenda sana kiasi kwamba alitoa uhai Wake ili tuweze kurudi kuishi na Mungu tena.
Pasaka Ni Kuhusu Upendo
Ni mara ngapi unaweza kupata neno upendo au kupendwa katika mistari hii? Andika idadi kwa kila andiko, kisha tafuta suluhisho la kihesabu. Unapopata jibu, jaribu kufanya vitu hivyo vingi kushiriki upendo wa Yesu na wengine.
Yohana 3:16
+
Yohana 1:34
+
Waefeso 5:2
-
Yohana 3:13
-
Warumi 8:35, 37
=