Liahona
Shindano la Uandishi wa Historia ya Kanisa
Machi 2026 Liahona


Shindano la Uandishi wa Historia ya Kanisa

Mwaliko wa Wasimulia Hadithi na Wanahistoria wa Eneo Husika kutoka Afrika na Ulaya

Unaalikwa kushiriki sauti yako katika Shindano la pili la Ulimwenguni la Historia ya Kanisa, linalodhaminiwa na Idara ya Historia ya Kanisa. Shindano hili linatafuta hadithi ambazo hazijasimuliwa za Watakatifu wa Siku za Mwisho wa Afrika na Ulaya kupitia masimulizi binafsi, historia za eneo husika, miradi ya vijana na tafiti za kielimu.

Waumini wote wenye umri wa miaka 16 na zaidi kutoka maeneo ya Afrika na Ulaya wanakaribishwa kuwasilisha. Zawadi za pesa taslim, fursa za uchapishaji na vyeti vya pongezi vinasubiri maingizo yatakayokidhi vigezo.

Ruhusu hadithi yako isikike. Saidia kuhifadhi utajiri na utofauti wa uzoefu ambao Watakatifu waliupitia.

Tarehe ya Mwisho ya Wasilisho: Julai 1, 2026
Muundo: Zilizoandikwa, sauti, au video

Tembelea ChurchofJesusChrist.org/learn/history/competition ili kujifunza zaidi na kuwasilisha ingizo lako.