“Huzuni yangu iligeuka kuwa shangwe,” Liahona, Machi. 2026.
Sauti za Watakatifu wa Siku za Mwisho
Huzuni Yangu Iligeuka kuwa Shangwe
Mtazamo mpya juu ya Upatanisho wa Yesu Kristo ulinisaidia kusonga mbele kwa imani na tumaini.
Kielelezo na Briana Kranz
Nilipokuwa na umri wa miaka 18, babu yangu upande wa mama yangu alifariki. Wakati huo katika maisha yangu, sikuwa nimempoteza mtu yeyote wa karibu nami. Nilijua ingetokea siku moja, lakini sikutarajia hilo litokee ghafla.
Babu yangu alikuwa na afya njema, lakini bila onyo, alipatwa na kiharusi. Bibi yangu haraka alimpeleka hospitalini, lakini alifariki siku nne baadaye.
Kumpoteza mtu ghafla kwa mara ya kwanza kunaumiza. Ilikuwa ajabu kuwa na babu yangu aliyehudhuria kila tukio muhimu katika maisha yangu na kisha ghafla anatoweka.
Baada ya mazishi, nilipata njia ya kuheshimu kumbukumbu ya babu yangu na muda wetu pamoja. Alipenda kufanya kazi kwenye lori lake na kufanya miradi mingine. Kwa kweli, alipoteseka kiharusi chake, alikuwa kwenye karakana yake akiwa ameshikilia spana katika moja ya mikono yake sugu, akifanya kazi kama kawaida.
Niliamua ningefanya kazi kwenye magari pia. Kufanya hivyo kunanisaidia kuhisi kuwa karibu naye. Pia niligeukia sala na maandiko, ambapo nilipata amani ya kusonga mbele kwa imani na tumaini katika kutokuwepo kwake.
“Kuna ufufuko,” nabii Abinadi ananikumbusha, “kwa hiyo kaburi halina ushindi, na uchungu wa kifo umemezwa katika Kristo” (Mosia 16:8).
Kifo cha babu yangu kilinisaidia kupata mtazamo ambao ulifanya Upatanisho wa Yesu Kristo kuwa wa maana zaidi katika maisha yangu. Kama vile tu nilivyomheshimu babu yangu kwa kufanya kazi kwenye magari, niligundua kwamba tunamheshimu Yesu Kristo—na kuweza kuhisi kuwa karibu Naye—tunapojitahidi kuishi kama Yeye alivyoishi, kujifunza injili Yake, kushiriki injili Yake, na kufanya “kazi ya Baba [Yake]” (Yohana 10:37). Kufanya hivyo kunatoa maana ya kina kwa Upatanisho wa Mwokozi na kuongeza imani yetu Kwake.
“Tunapolia kwa huzuni au shangwe, Yesu Kristo anaelewe kikamilifu,” Mzee Gerrit W. Gong wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alifundisha. “Yeye anaweza kuwa yupo katika nyakati ambazo tunahitaji zaidi zawadi kuu za milele: Upatanisho wa Yesu Kristo, Ufufuko, urejesho.”
Yesu Kristo amegeuza huzuni yangu kuwa shangwe. Kwa sababu Yake na Upatanisho Wake, ninajua nitamwona babu yangu tena.