Liahona
Watumishi Wenye Haki—Wanafunzi wa Yesu Kristo
Machi 2026 Liahona


“Watumishi wenye Haki—Wanafunzi wa Yesu Kristo,” Liahona, Machi 2026.

Wanawake wa Agano

Wafuasi Wenye Haki—Wanafunzi wa Yesu Kristo

Mifano mitatu inafundisha usimamizi na kuonyesha jinsi ya kuongeza kina cha uanafunzi wetu kwa Yesu Kristo.

kielelezo cha mfano wa wanawali kumi.

Wanawali Kumi, na Jorge Cocco

Kuruhusu nuru ya Yesu Kristo iangaze katika uanafunzi wetu ni aina ya msingi ya nishati mbadala—nishati kutoka chanzo ambacho kinajazwa kila mara. Kwa kuleta faraja na nuru ya Kristo kwa wengine, tunapata faraja yetu wenyewe katika Yeye.

Kwa hiyo kuwa mpatanishi katika nyumba yako mwenyewe na jamii na katika uwepo wako mtandaoni. Punguza mateso katika ujirani wako mwenyewe.

Lengo la Shetani ni kwamba tutendewe. Kinyume chake, mpango wa furaha wa Baba unatupa fursa ya kutenda, kuwa mawakala kwa ajili ya mema, amani, tumaini.

Tunaweza kukabiliana na upotoshaji kwa kushiriki habari za kuinua, zenye matumaini, na sahihi, kwa kuwa watetezi wa ukweli badala ya watumiaji wa habari tu. Tunaweza kujibu uovu kwa kuujaza ulimwengu kwa nuru na habari njema ya injili ya Yesu Kristo.

Kama nabii wetu mpendwa, Rais Russell M. Nelson, amesema, jibu daima ni Yesu Kristo: “Maswali au matatizo yoyote uliyonayo, jibu daima linapatikana katika maisha na mafundisho ya Yesu Kristo.”

Rais Nelson ametualika kufanya uanafunzi wetu Kwake kuwa “kipaumbele chetu cha juu.” Tunaongeza kina cha uanafunzi wetu tunapojifunza kutoka kwa Yesu Kristo na kuhusu Yesu Kristo. Kwa hiyo, acha tuchunguze mafundisho ya Mwokozi.

Wanawali Kumi

Mathayo 25 ina mifano mitatu inayosimulia. Kwanza, mfano wa wanawali kumi (ona mistari ya 1–13). Watano walikuwa wenye busara na watano walikuwa wapumbavu. Wote kumi walikuwa katika eneo sahihi, wakimsubiri bwana harusi, na kila mmoja alikuja na taa.

Wakati bwana harusi—akimwakilisha Mwokozi—alikuja bila kutegemewa usiku wa manane, wanawali watano hawakuwa na mafuta ya kutosha kwa ajili ya taa zao. Pengine walifikiri kuwa na mafuta ya ziada haikuwa ya lazima. Au huenda hawakuwa wasimamizi wenye busara wa mafuta waliyokuwa nayo. Labda vivuruga mawazo, walishindwa kujitayarisha vya kutosha kuweka taa zao zikiwaka.

Na hivyo, katika kujibu ombi lao la kuingia kwenye karamu ya harusi, bwana harusi alijibu, “Hamnijui” (Tafsiri ya Joseph Smith, Mathayo 25:11 [katika Mathayo 25:12, tanbihi a]). Kinyume chake, hii inamaanisha kwamba kupitia maandalizi yao na usimamizi wenye busara, wanawali watano wenye busara walimjua Yeye.

Mafuta ya thamani yanaweza kuonekana kama uongofu wao binafsi. Iliwaruhusu wanawali wenye busara kuangaza taa zao na kuingia kwenye karamu ya ndoa pamoja na bwana harusi. Mafuta hayangeweza kugawanywa kwa marafiki zao kwa sababu uongofu wa mtu ni—wa kibinafsi. Tunaweza na tunapaswa kushikilia nuru ya taa zetu juu ili kuinua na kuimarisha na kupungia mkono wengine kwa Yesu Kristo, lakini kila mmoja wetu ni mtumishi wa uongofu wetu wenyewe.

Kama ilivyoelezwa na Mwokozi, “Kuweni waaminifu, na mkisali daima, mkitengeneza na kuziwasha taa zenu mkiwa pamoja na mafuta yake, ili kwamba muweze kuwa tayari Bwana harusi ajapo” (Mafundisho na Maagano 33:17; msisitizo umeongezwa).

Talanta

Mfano wa pili uliosemwa katika Mathayo 25 ni ule wa talanta (ona mistari 14–30). Katika hadithi ile, bwana, kwa matarajio ya kusafiri mbali, aliwapa watatu kati ya watumishi wake talanta. “Talanta” iliwakilisha fedha. Tunaweza pia kufikiria juu ya hizo kama karama, uwezo, na baraka kutoka kwa Baba yetu wa Mbinguni. Kwa mtumishi mmoja bwana alimpa talanta tano, kwa mwingine talanta mbili, na kwa watatu alimpa talanta moja. Na kisha bwana akasafiri.

Aliporudi, aligundua kwamba watumishi ambao alikuwa amewapatia talanta tano na talanta mbili walikuwa wasimamizi waaminifu na wenye faida na walikuwa wamefanya matumizi mazuri ya talanta zao wakiongeza mara mbili thamani yake. Na baada ya kuwa waaminifu juu ya kidogo,bwana aliwapa zaidi akisema, “Vema, mtumishi mwema na mwaminifu: umekuwa mwaminifu katika mambo machache, nitakufanya kuwa mtawala juu ya mambo mengi; ingia katika furaha ya Bwana wako (Mathayo 21).

Kinyume chake, mtumishi mwenye talanta moja aliizika—pengine kwa sababu alivurugwa mawazo na kuahirisha. Au labda alifadhaika kwa kujua jinsi ya kuanza au kuogopa kwamba angeshindwa. Pengine alijifananisha na watumishi wengine, na shaka zake zilimzuia kujaribu. Hakuwa amejiandaa kwa ajili ya kurudi kwa bwana, hakupata uzoefu wa furaha ya usimamizi mwaminifu, na alipoteza talanta yake.

Mfano wa wanawali kumi na mfano wa talanta ni sambamba. Yote yanasisitiza kwamba tuna jukumu binafsi kwa uongofu wetu na lazima tujitayarishe kupokea kipawa cha Bwana cha kuinuliwa—na kwamba tuna utumishi na uwajibikaji binafsi kwa vipaji na karama tulizopewa.

Kondoo wa Mchungaji Mwema

Hatimaye, Mathayo 25 inaelezea hadithi ya wale ambao “wanajiamini mbele ya Mungu,” wakielezewa kama kondoo wa Mchungaji Mwema, wanaopatikana upande Wake wa kulia, wakifurahia karamu ya harusi pamoja Naye, na kubarikiwa kuwa watawala juu ya mambo mengi (ona mstari wa 31–40). Bwana atawaambia:

“Nilikuwa na njaa, mkanipa chakula: nilikuwa na kiu, mkaninywesha: nilikuwa mgeni, mkanikaribisha:

“Uchi, mkanivika, nilikuwa mgonjwa, mkaja kunitembelea: nilikuwa kifungoni, na mlikuja kwangu” (Mathayo 25:35–36).

Kama wanafunzi Wake, tunajitayarisha wenyewe kwa Ujio Wake wa Pili na kwa uaminifu na kwa faida tunafanya usimamizi juu ya yale ambayo tumebarikiwa nayo. Huruma, hisani, wema, na utumishi wa uaminifu hutustahilisha si tu kuishi naye baadaye bali pia kuwa na kujiamini mbele ya Mungu sasa. Kama Mormoni alivyofundisha, kwa wale ambao wamejawa na hisani—upendo msafi wa Kristo—“itakuwa vyema [kwao]” katika siku ya mwisho. Watakuwa kama Mwokozi, wakimwona yeye kama Alivyo na kujazwa na tumaini na kutakaswa hata kama vile Yeye alivyo safi. (Ona Moroni 7:47–48). Rais Nelson ametangaza, “Hisani na wema hufungua njia ya kuwa na kujiamini mbele za Mungu!”

kielelezo cha mtu aliyebeba mwanakondoo

Shepherd—Variation IV, na Jorge Cocco

Wanafunzi wa Yesu Kristo huwajali wale walio katika shida .

Mifano hii yote mitatu inafundisha usimamizi wa uongofu wetu wenyewe; kwa ajili ya karama, talanta, na mali ambazo tumebarikiwa nazo; na kwa majirani zetu ambao wana njaa, wasio na makazi, wanaoumizwa, na waliochoka.

Inafundisha jinsi wanafunzi wa Kristo wanavyopaswa kujiandaa kwa nyakati za hatari ambazo zitatangulia Ujio wa Pili wa Mwokozi. Hizi ndizo nyakati tunazoishi! Tunapaswa kuweka taa za uongofu wetu zikiwaka kwa uangavu, kuacha nuru yetu iangaze, tukitumia na kupanua talanta zetu, na kuwajali wale wenye uhitaji. Hii ni kuwa na hisani, upendo msafi wa Kristo.

Mihutasari

  1. Russell M. Nelson, “Jibu Daima ni Yesu Kristo,” Liahona, Mei 2023, 127.

  2. Russell M. Nelson, “Bwana Yesu Kristo Atakuja Tena,” Liahona, Nov. 2024, 121.

  3. Mzee David A. Bednar wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alifundisha kwamba tuna “jukumu binafsi la kuweka taa yetu ya ushuhuda kuwaka na kupata akiba ya kutosha ya mafuta ya uongofu. Mafuta haya ya thamani yanapatikana tone moja baada ya jingine—‘mstari juu ya mstari [na] kanuni juu ya kanuni’ (2 Nefi 28:30), kwa subira na kwa kusonga bila kuchoka. Hakuna njia ya mkato; wasiwasi wa maandalizi ya dakika ya mwisho hayafui dafu” (“Kuongoka kwa Bwana,” Liahona, Nov. 2012, 109).

  4. Russell M. Nelson, “Kujiamini katika Uwepo wa Mungu,” Liahona, Mei 2025, 127.

  5. Rais Russell M. Nelson, “Kujiamini katika Uwepo wa Mungu,” 128.