Liahona
Mwongozo wa Agano la Kale wa Kukumbatia Utambulisho wa Kiungu
Machi 2026 Liahona


“Mwongozo wa Agano la Kale wa Kukumbatia Utambulisho wa Kiungu,” Liahona, Mar. 2026.

Kutoka VW Kila Wiki

Mwongozo wa Agano la Kale wa Kukumbatia Utambulisho wa Kiungu

Watu katika Agano la Kale yawezekanakuwa walikabiliana na baadhi ya maswali sawa na yale ambayo mimi na wewe tunaweza kuwa nayo leo.

Yesu Kristo akitazama anga la usiku

Hapo Mwanzo Kulikuwa na Neno, na Eva Timothy, linaweza kunakiliwa kwa ajili ya matumizi ya Kanisa pekee

Nitakuwa naongopa kama ningekuambia kamwe sijawahi kutilia shaka jukumu langu katika mpango wa Mungu.

Jinsi gani ningeweza—nisivyo mkamilifu kama nilivyo—kuweza kutosha katika mpango Wake mkamilifu? Ni kwa jinsi gani ninaweza kuwa mwenye kustahili nafasi ya pili Ambayo Baba wa Mbinguni hunipa muda baada ya muda? Jinsi gani ningeweza kuaminiwa kushiriki upendo Wake pamoja na wengine wakati mwingine ninahangaika kuusikia upendo huu mimi mwenyewe?

Kama mzunguko huu wa kifo unaonekana kufahamika, hauko peke yako.

Mojawapo ya mbinu kubwa ya adui ni kushambulia uelewa wetu wa utambulisho wa kiungu. Mzee Brian K. Taylor wa sabini alifundisha, “Vita hii kuu kuhusu utambulisho wa kiungu inaendelea kwa nguvu huku silaha za Shetani zinazoenea zikilenga kuharibu imani yetu katika na ufahamu wetu kuhusu uhusiano baina yetu na Mungu.”

Kwa bahati nzuri, Baba wa Mbinguni amefundisha—na anaendelea kufundisha—watoto Wake kuhusu thamani yao. Tangu mwanzo kabisa, watu katika maandiko waliweza kuwa wamekabiliana na baadhi ya maswali yale yale ambayo mimi na wewe tunaweza kuwa nayo leo.

Unapojifunza Agano la Kale mwaka huu, unaweza kujifunza kuhusu utambulisho wako mwenyewe wa kiungu kwa kutumia uzoefu wa watu katika maandiko kwenye maisha yako mwenyewe. Na pengine utapata majibu kwa kila swali muhimu sana muda wote

“Mimi ni Nani?”

Mimi ni …

Kukabidhiwa Usimamizi Mtakatifu

Adamu na Hawa wanaweka alama mwanzo kabisa wa hitaji la mwanadamu kuelewa utambulisho wa kiungu. Baba wa Mbinguni aliwaumba kwa mfano Wake mwenyewe, aliwapa usimamizi juu ya dunia na viumbe vyote juu yake, na akawaamuru kuongezeka na kuijaza dunia (ona Musa 2:26–28).

Kama uzao wa Adamu na Hawa, unaweza kutumia kanuni hizi hizi za utambulisho kwako mwenyewe. Wewe ni mtoto halisi wa kiroho wa Mungu mwenye jukumu la kiungu la kutenda kama msimamizi mwenye busara na kujenga familia ya milele.

Wakati Adamu na Hawa walipokula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya, walitupwa nje ya Bustani ya Edeni. Ingawa walitengwa kutoka uwepo wa Baba wa Mbinguni, kimwili na kiroho, Yeye aliwapatia Mwokozi ili kuwasaidia kushinda vyote kifo cha kimwili na kiroho kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo.

Kama Adam na Hawa, thamani yako ni “kuu mbele za Mungu” (Mafundisho na Maagano 18:10).

Mimi ni …

Mtoto wa Agano la Ibrahimu

Hadithi ya Ibrahimu imefungwa moja kwa moja na utambulisho wa kiungu. Bwana alitoa ahadi ya matokeo ya milele kwa Ibrahimu:

“Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nami nitakubariki, na kulifanya jina lako kuwa kubwa; nawe utakuwa baraka:

“Na nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani: na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa” (Mwanzo 12:2–3).

Baada ya miaka mingi ya kusubiri kwa imani, Ibrahimu na Sara walibarikiwa kwa kuzaliwa kwa mwana wao, Isaka. Mungu kisha akamwamuru Ibrahimu kumtoa dhabihu “mfano wa Mungu na Mwanawe wa Pekee” (Yakobo 4:5). Wakati Ibrahimu alipoonyesha alikuwa tayari kufanya dhabihu kama hiyo, alisimamishwa na malaika wa Bwana.

Tunasoma:

Nimeapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwa kuwa umetenda hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee:

Katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;

“Na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu” (Mwanzo 22:16–18).

Hadithi hii yenye nguvu inafundisha kwamba wote wanaofanya na kushika maagano na Baba wa Mbinguni wanaweza kupata baraka zilizoahidiwa kwa uzao wa Ibrahimu. Kama mtoto wa agano, unaweza kupokea baraka zilizoahidiwa za agano la Ibrahimu kwa kushikilia ahadi unazofanya na Bwana kupitia maagano ya ubatizo au hekaluni.

Mimi ni …

Mwanafunzi imara wa Bwana

Hajiri—Mjakazi wa Sara na mama wa Ishmaeli—anafundisha uwezo wetu wa kuvutia wa uthabiti. Kufuatia kuzaliwa kwa Isaka, mwana wa Ibrahimu na Sara, Hajiri na Ishmaeli walihamishwa kwenda jangwani (ona Mwanzo 21:9–14).

Akiona dhiki yake na maombi ya dhati kwa ajili ya maisha ya Ishmaeli, Bwana alimtuma malaika kumfariji: “Usiogope; kwani Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko. Ondoka, ukamwinue kijana, na ukamshike mkononi mwako; kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa” (Mwanzo 21:17–18).

Hata wakati Hajiri alipohisi kuwa peke yake jangwani, Baba wa Mbinguni hakumwacha. Alilindwa na kuzawadiwa kwa imani na bidii yake.

Kama Hajiri, unaweza kuhisi kama unatangatanga jangwani peke yako. Lakini wewe ni wa thamani kubwa kwa Baba yako wa Mbinguni. Unaweza kutangatanga jangwani kwa muda, lakini Yeye hajakusahau. Anakutayarisha kufanya mambo makuu kwa ajili ya kujenga ufalme Wake.

Mimi ni …

Mikono ya Mungu Duniani

Musa aliitwa na Baba wa Mbinguni kuwakomboa Waisraeli kutoka utumwani Misri. Alifanya mfululizo wa miujiza yenye nguvu ambayo hatimaye iliongoza kutoroka kwao (ona Kutoka 7; 14).

Ingawa alifanikiwa katika wito wake, Musa hakuwa daima mwenye kujiamini katika uwezo wake wa kufanya kama Baba wa Mbinguni alivyomwamuru. Wakati Musa alipoelezea hisia zake za kutotosha, Bwana alijibu, “Bila shaka mimi nitakuwa pamoja nawe; na dalili ya kuwa nimekutuma ndiyo hii: utakapokuwa umekwisha kuwatoa hao watu katika Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu” (Kutoka 3:12).

Musa alikumbatia utambulisho wake kama mtoto wa Mungu na alipata nguvu za Baba wa Mbinguni ili kufanya miujiza Yake. Kama Musa, unaweza kupata nguvu ya kufanya kazi ya Mungu unapokumbatia uhusiano wako wa milele na Baba wa Mbinguni.

Mimi ni …

Kwa hiyo, Wewe ni nani?

Sasa ni wakati wa wewe kugundua jibu kwa ajili yako mwenyewe.

Pekua maandiko kwa ajili ya majibu ya maswali yako, na utayapata. Baba wa Mbinguni anakutaka uelewe wewe ni nani hasa ili uweze kujipenda kama Anavyokupenda.

Maarifa ya utambulisho wako wa milele, wa kiungu yako karibu tu—kwa hivyo unasubiri nini?