2025
Kagua Lango
Machi 2025


“Kagua Lango,” Liahona, Machi 2025.

Sauti za Watakatifu wa Siku za Mwisho

Kagua Lango

Wakati nikihudumu kwenye shamba la mifugo, nilijifunza somo la thamani kuhusu daima kufuata misukumo kutoka kwa Roho Mtakatifu.

watu wawili wakizungumza katika jengo la mifugo kwa ajili ya farasi

Picha ya mwandishi kwenye ranchi na Shaun Sutton

Karibu na mwisho wa muda wangu kama mmisionari kijana wa huduma, nilifuata msukumo wa kuhudumu siku mbili kwa wiki katika shamba la mifugo la utalii huko Utah kwa familia za wanajeshi na walio nusurika. Nilikuwa na uzoefu sifuri kabisa wa kitu cho chote hata kinachohusiana na shamba la mifugo, lakini nilikuwa na shauku.

Mapema katika wakati wangu huko, niliombwa kusafisha banda la farasi. Rafiki yangu mwema na mwenzangu ambaye nilikwenda naye kufundisha jioni, Mzee Saltern, alipangiwa kunionyesha nini cha kufanya.

Nikifikia banda la mwisho kusafisha siku moja, nilimfuata Mzee Saltern ndani. Katika akili yangu nilipokea msukumo mpole wa kuuliza kuhusu kufunga lango nyuma yetu. Nilipuuzia mbali wazo hilo na nikaenda kufanya kazi ya kusafisha.

Farasi katika lile banda, Shrek, alikuwa mmoja wa farasi mkubwa zaidi katika ranchi. Alianza kuhama kwa wasiwasi tulipokuwa tukisafisha. Ghafla, Shrek alitoka nje ya banda kupitia lango lililo wazi na kukimbia kupita farasi wengine nje katika matumbawe.

Kwa shukrani, mmoja wa watu wenye uzoefu katika ranchi alichukua ndoo ya unga na haraka akamrudishia yule farasi. Alipokuwa akimrudisha Shreki ndani ni banda lake, alinitazama na kuniuliza kwa kushangaa, ”Tulijifunza nini?”

Somo la wazi lilikuwa daima kufunga lango. Nilikumbushwa maandiko niliyokuwa nimesoma asubuhi ile ambayo yalinifundisha kukubali “ushawishi wa Roho Mtakatifu” (Mosia 3:19).

Wakati mimi na Mzee Saltern tulipoingia katika banda la Shrek, nilikuwa nimepuuza msukumo kutoka kwa Roho Mtakatifu wa kufunga lango. Nilikuwa nimempanga Roho katika kunishauri tu juu ya kile nilichofikiria ni vitu vya “kiroho” vinavyohusiana na maandiko au amri. Tukio hili lilininyenyekeza. Niligundua kwamba maarifa ya Roho yalikuwa makubwa kuliko nilivyotambua—hata inapokuja kwenye ranchi!

Rais Thomas S. Monson (1927–2018) alifundisha, “Kumbuka kwamba kazi hii si yenu na yangu peke yangu. … Tunapokuwa katika kazi ya Bwana, tunastahili usaidizi wa Bwana.”

Yawezekana nisingekuwa nafundisha injili kwenye ranchi, kama ambavyo ningefanya jioni hiyo pamoja na Mzee Saltern, lakini nilistahili usaidizi wa kiungu na mwongozo—hata wakati nikisafisha mabanda ya farasi.