2025
Urejesho wa Sakramenti
Machi 2025


“Urejesho wa Sakramenti,” Liahona, Machi 2025.

Njoo, Unifuate

Mafundisho na Maagano 20; 27

Urejesho wa Sakramenti

sakramenti ikipitishwa katika muundo wa Kanisa la urejesho

Wakati Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ilipoanzishwa mnamo 1830, Bwana alirejesha ibada takatifu ya sakramenti. Aliwaamuru watu Wake “kukutana pamoja mara kwa mara ili kupokea mkate na divai katika ukumbusho wa Bwana Yesu” (Mafundisho na Maagano 20:75).

Ratiba hii inaonyesha jinsi sakramenti ilivyoanzishwa katika zama tofauti. Ingawa watu na mahali hubadilika, katika kila zama sakramenti huwasaidia wanafunzi wa Yesu Kristo daima kumkumbuka na kuwa na Roho Wake pamoja nao.

Agano Jipya

Kitabu cha Mormoni

Mafundisho na Maagano

Siku yetu

Wakati Yesu Kristo atakapokuja tena

Ambao

Yesu Kristo na wanafunzi Wake huko Yerusalemu

Yesu Kristo na Wanefi

Joseph Smith na waumini wa kwanza wa Kanisa la urejesho la Yesu Kristo

Watakatifu wa Siku za Mwisho ulimwenguni kote

Yesu Kristo na “wale wote ambao Baba [Yake] amempa [Yeye] kutoka ulimwenguni” (Mafundisho na Maagano 27:14)

Nini

Mkate na divai kwa ukumbusho wa mwili na damu ya Yesu (ona Mathayo 26:26–28; Marko 14:22–24; Luka 22:17–20)

Mkate na divai kwa ukumbusho wa mwili na damu ya Yesu (ona 3 Nefi 18)

Mkate na divai, vikibarikiwa kwa sala mahususi zinazopatikana katika Mafundisho na Maagano 20:77, 79

Kwa kawaida mkate na maji, vikibarikiwa kwa sala maalum zinazopatikana katika Mafundisho na Maagano 20:77, 79

Mkusanyiko ulioongozwa na Yesu Kristo, ambapo Yeye “atakunywa matunda ya mzabibu pamoja [nasi] duniani” (Mafundisho na Maagano 27:5)

Lini

Ilianza karibia miaka 33 B.K, usiku ule kabla ya Kusulubiwa kwa Yesu Kristo

Ilianza karibia miaka 33 B.K baada ya Ufufuko wa Yesu Kristo

Ilianza wakati Kanisa lilipoanzishwa Aprili 6, 1830 …

Kila wiki katika mikutano ya sakramenti

Wakati Yesu Kristo anapokuja tena duniani

Wapi:

Katika “chumba kikubwa orofani” cha nyumba iliyoko Yerusalemu (Marko 14:15)

Katika “nchi ya Neema” (3 Nefi 11:1)

Katika nyumba ya Whitmer huko Fayette, New York, Marekani

Katika nyumba za mikutano ulimwenguni kote

“Duniani” (Mafundisho na Maagano 27:5)

Kwa nini

Kuwapa watu nafasi ya kumkumbuka Yesu Kristo na “kufanya upya agano lao la kujichukulia juu yao jina la Mwokozi, ili daima kumkumbuka Yeye, na kushika amri Zake.”

Tafakari

Ni kwa jinsi gani kujua lengo la sakramenti kunaimarisha uhusiano wako na Yesu Kristo?

Mihutasari

  1. Yesu Kristo alianzisha sakramenti miongoni mwa wanafunzi Wake huko Yerusalemu wakati wa sherehe za mwaka za Pasaka, ambayo inajumuisha mlo wa ishara ya mkate ili kukumbuka kwamba Mungu aliwakomboa Waisraeli kutoka Misri (ona Marko 14:12; ona pia Kutoka 12:17). Rais Jeffrey R. Holland, Kaimu Rais wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili, aliuliza, “Je, tunaona [ibada yetu ya sakramenti ya kila wiki] kama pasaka yetu, ukumbusho wetu wa usalama, ukombozi na wokovu? … Unapaswa kuwa wakati wenye nguvu, wakati wa unyenyekevu, na wa kutafakari” (“This Do in Rembrance of Me,” Ensign, Nov. 1995, 68).

  2. Kitabu cha Maelekezo ya Jumla: Kuhudumu katika Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za Mwisho, 29.2.1, Maktaba ya Injili.