Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana
Aliuzwa Misri
Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana Machi 2026


Hadithi kutoka Agano la Kale

Mwanzo 37–47

Aliuzwa Misri

Yusufu

Aliuzwa Misri

Pakua PDF

Vielelezo na Katy Dockrill

Hadithi Yake

Koti

Yusufu alikuwa mtoto mpendwa wa Yakobo. Yakobo alimtengenezea Yusufu koti maalum. Kaka zake Yusufu walimwonea wivu. (Haikuwapendeza kwamba Yusufu alioteshwa ndoto zilizokuwa na mwongozo wa kiungu kutoka kwa Mungu kwamba siku moja angewatawala.)

Usaliti

Kaka zake Yusufu walimuuza kwa watu waliokuwa wakienda Misri na kumwambia Yakobo kwamba Yusufu alikuwa amefariki. Huko Misri, Yusufu alikuwa mtumwa na alitupwa gerezani kwa kosa ambalo hakufanya. Daima alikuwa mwaminifu kwa Mungu, na Bwana alikuwa pamoja naye na akambariki.

Baa la Njaa

Hatimaye, Yusufu alitafsiri ndoto ya Farao na kumpa ushauri wa kujiandaa kwa ajili ya njaa ijayo. Farao alimfanya Yusufu kuwa mtawala huko Misri. Punde, kaka zake walikuja Misri kununua nafaka. Hawakutambua kuwa walikuwa wakiomba msaada kutoka kwa ndugu waliyekuwa wamemuuza!

Ukombozi

Yusufu hatimaye alijifunua mwenyewe kwa kaka zake na kuwapa chakula na makazi huko Misri. Aliwasamehe na kuokoa familia yake. Kaka hawa hawa wakawa makabila 12 ya Israeli.

Hadithi Yako

Kama Yusufu, unaweza kuwa na siku ambazo unahisi kusalitiwa au kuumizwa. Matendo ya watu wengine yanaweza kuwa na matokeo makubwa. Lakini unapokuwa mwaminifu kwa Mungu na kujaribu kuwasamehe wengine, utaimarishwa na kubarikiwa.