Kwenye Hoja
Ni kwa jinsi gani tunaishi katika ulimwengu na “kuweka kando mambo ya ulimwengu huu”?
Wanafunzi Ambao Alikuwa Amewachagua, na Casey Childs
Bwana amesema, “Nawe utayaweka kando mambo ya ulimwengu huu, na kuyatafuta mambo ya ulimwengu ulio bora” (Mafundisho na Maagano 25:10). Hii haimaanishi kwamba tunapuuza mahitaji na nyenzo zetu za kimwili, lakini inamaanisha kwamba hatuwezi kuweka mioyo yetu juu ya utajiri, mamlaka, cheo, au kukubalika na ulimwengu. Hapa kuna baadhi ya kanuni ambazo tumefundishwa kuhusu kuishi ulimwenguni:
Weka mambo ya Mungu kwanza. “Tafuteni kwanza ufalme na Mungu, na haki yake” (Mathayo 6:33). Katika mioyo yetu na maisha yetu, amri za Mungu na maagano yetu na Yeye ni kipaumbele chetu.
Tafuteni Maarifa. “Unapojifunza kuhusu ulimwengu unaokuzunguka, jifunze pia kumhusu Mwokozi. … Kadiri unavyojifunza zaidi, ndivyo unavyoweza kusaidia kujenga ufalme wa Mungu na kuushawishi ulimwengu kwa mema” (Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana: Mwongozo wa Kufanya Chaguzi [2022], 31, 32).
Kazi. “ Kazi ni kanuni muhimu ya Injili. Inachochea ukuaji na kutuendeleza sisi. … Bwana siyo tu hataki tutoe mahitaji kwa ajili ya familia zetu bali ‘kujishughulisha kwa shauku katika kazi njema’ [Mafundisho na Maagano 58:27]” (“Ajira,” Mada na Maswali, Maktaba ya Injili).