2025
Kusonga pamoja na Roho
Machi 2025


Kusonga pamoja na Roho

Baba wa Mbinguni anataka kuzungumza nawe. Hapa kuna njia unazoweza kufanya mawasiliano hayo yaendelee.

mvulana akisali

Baba yako wa Mbinguni anakujua na anakupenda. Anakusikia wakati unaposali, na Anataka kuzungumza nawe. Kugundua jinsi Yeye anavyozungumza ni muhimu—na ni tofauti kwetu sote. Lakini mara nyingi, unaweza kumwona Baba wa Mbinguni akizungumza akilini na moyoni mwako wakati unapokuwa unasonga—kuishi maisha yako na kutenda kwa imani.

Baki Umeunganika

Unaweza kuweka muunganiko wako na Baba wa Mbinguni wazi wakati unaposali Kwake mara kwa mara na kwa dhati. Jifunze neno Lake katika maandiko. Wasikilize na uwafuate watumishi Wake wateule—manabii na mitume. Unaweza kufanya kadiri uwezavyo kutii amri zake.

Kubakia umeunganika na Baba wa Mbinguni kunaleta furaha na maana kwenye maisha yetu. Kunatusaidia tuelewe vyema mpango Wake na kuhisi upendo Wake. Tunatambua anapozungumza kadiri tunapojitahidi kubaki katika hali ya juu ya kiroho.

kijana akiangalia upeo wa macho

Tulia

Kumbuka ushauri huu kutoka kwa Bwana: “Tulieni na jueni kuwa Mimi ni Mungu” (Zaburi 46:10; ona pia Mafundisho na Maagano 101:16). Ulimwengu umejawa na kelele na vivuruga usikivu, lakini Baba wa Mbinguni sio mwenye sauti kubwa au mwenye kelele. Anazungumza katika “sauti ndogo tulivu” (1 Wafalme 19:12). Tunaweza kutambua ushawishi Wake wakati tukiwa watulivu.

Kwa mfano, tafuta mahali pa utulivu ili usali, pata muda wa kujizingira kwa uzuri wa uumbaji wa Mungu katika mazingira ya asili, au furahia muziki na sanaa ya kuvutia. Mambo haya husaidia kuweka akili zetu na mioyo yetu kuwa wazi kwa uzoefu maalumu na Baba wa Mbinguni.

msichana

Fuata Misukumo ya Kiroho

Baba wa Mbinguni mara nyingi huzungumza nasi kupitia misukumo ya kiroho. Lakini tunawezaje kujua kwa uhakika kama msukumo wa kiroho unatoka Kwake? Nabii Mormoni anatupatia mwongozo mzuri: “Kila kitu kinachokaribisha na kushawishi kufanya mema, na kumpenda Mungu, na kumtumikia, kinaongozwa na Mungu” (Moroni 7:13). Rais Gordon B. Hinckley (1910–2008) aliwahi kusema: “Hilo ndilo jaribio, wakati yote yanaposemwa na kufanywa. Je, kinamshawishi mtu kufanya mema, kuinuka, kusimama wima, kufanya jambo sahihi, kuwa mpole, kuwa mkarimu? Basi huo ni ushawishi wa Roho wa Mungu.”

Mara nyingi, msukumo wa kiroho utakuwa “nenda na kutenda” (ona 1 Nefi 3:7) au kusema kitu fulani. Tunapotenda kulingana na msukumo huo—hasa mara ya kwanza tunapouhisi—uzoefu zaidi utakuja. Kwa hiyo, kama unahisi kwamba unapaswa kusema au kufanya kitu kizuri na chanya, fanya hivyo! Uthibitisho kwamba uko kwenye njia sahihi huja wakati unapofanya hivyo.

vijana

Songa Mbele kwa Imani na Tumaini

Kutambua wakati Mungu anapozungumza ni mchakato. Inahitaji vyote imani na tumaini kwamba Baba wa Mbinguni atazungumza nawe na kukusaidia ufanye zaidi kuliko unavyoweza kufanya wewe mwenyewe. Ni muhimu pia kukumbuka kwamba Baba wa Mbinguni anakutumaini wewe sio tu kutafuta mwongozo Wake katika maisha yako mwenyewe bali pia kuwabariki na kuwainua wale walio karibu nawe.

Hutakuwa na majibu yote kila mara. Hautarajiwi kuwa nayo yote. Lakini. Unahimizwa kutenda kwa imani. Unapofanya hivyo, utagundua kwamba Mungu anaweza kuzungumza kwa njia nyingi kuliko unavyoweza kufikiria. Baada ya muda, sauti Yake itakuwa wazi zaidi, mwongozo Wake utaonekana zaidi, na uwepo Wake utaonekana zaidi kukusaidia kuwa kile Anachojua unaweza kuwa.