Siri ya Kutoanguka Tena
Ni rahisi zaidi kuliko unavyofikiri.
Vielelezo na Eric Chow
“Ninapenda kushindwa!”
Hiyo labda sio kitu ambacho umesikia watu wengi wakisema. Wengi wetu hatufurahii kuhusu kushindwa. Inaweza kuumiza, kutupilia mbali mipango yetu, na wakati mwingine kuleta aibu kabisa.
Lakini vipi kama kulikuwa na siri ya kutoshindwa tena?
“Ngoja,” unaweza kuwa unafikiria. “Hakuna aliye mkamilifu. Sisi sote tunafanya makosa. Ni kwa jinsi gani mtu hawezi kushindwa?”
Thomas Edison aligundua siri wakati akijaribu mara nyingi kuvumbua balbu ya mwanga. “Sikushindwa mara 1,000,” inasemekana alisema. “Taa ya balbu ni uvumbuzi wa hatua 1,000.”
Edison alishindwa tena na tena, lakini hakuchagua kuiona kwa njia hiyo. Na hiyo ndiyo siri! Hamisha mtazamo wako! Unapohamisha mtazamo wako, “kushindwa kwako” kunaweza kuwa kitu kipya na chanya.
Hapa ni njia nne za kubadilisha mtazamo wako kuhusu kushindwa:
-
Tafuta kile unachoweza na usichoweza kudhibiti. Wakati mwingine vitu tunavyovihofia vingi havipo katika udhibiti wetu. Chukulia kuomba kazi, kwa mfano. Wewe unaweza kudhibiti juhudi unazoweka katika kuomba kazi, lakini wewe huwezi kudhibiti matokeo. Badala ya kutumia nguvu ukihofu kwamba “utashindwa,” jaribu kuweka juhudi katika kile ulicho na udhibiti nacho na kumwamini Bwana. Ameahidi kwamba “Mambo yote yatafanya kazi pamoja kwa faida ya wale wampendao Mungu” (Warumi 8:28). Na kama hutapata kazi hiyo? Wewe siyo mshindwaji! Hata kama hupati matokeo uliyokuwa unayategemea, ulitoa juhudi zako bora, na hayo ni mafanikio!
-
Nyakua mema na endelea na mwendo Unapohisi kama unashindwa, jaribu kuangalia kwa kina zaidi kwenye uzoefu wako. Hukufanikiwa kuwa katika timu ya michezo? Ulipata alama za kuvunja moyo kwenye jaribio? Kuangalia mahali ambapo ulihangaika kutakupa ramani kubwa kwenye kile unachohitaji kufanya katika siku zijazo. Kama uzoefu unakufanya ujisikie mwenye thamani ndogo, tambua hisia zako na kisha chagua kuendelea na wema. Kushindwa kunaweza hakika kukusaidia kuendelea mbele katika mwelekeo mpya na ulio bora.
-
Kumbuka huu sio mwisho. Kuna msemo wa kawaida: “Kila kitu kitakuwa sawa mwishoni. Kama sio sawa, sio mwisho.” Moroni anafundisha kitu kama hicho. Alisema “Je, mwisho umefika? Tazama nawaambia, Hapana; na Mungu hajakoma kuwa Mungu wa miujiza” (Mormoni 9:16). Tunapomwamini Mungu, na tusonge mbele kwa imani, na kukumbuka kwamba hadithi zetu hazikomi wakati kitu kinapokwenda vibaya, miujiza inaweza kutokea na “kushindwa” kokote tunakoweza kukabiliana nako hatimaye kunaweza kuwa mafanikio ya kupendeza.
-
Simama na Kristo. Kwa sababu ya Upatanisho wa Yesu Kristo, hakuna kushindwa ambako ni kwa kudumu. Daima tuna chaguo la kutubu, kugeuza mioyo yetu kurudi kwa Mungu, na kuomba msaada Wake. Rais Jeffrey R. Holland, Kaimu Rais wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili, amefundisha: “Licha ya makosa mengi unayohisi umeyafanya … , Ninakushuhudia kwamba haujasafiri kupita ufikiaji wa upendo wa kiungu. Haiwezekani kwa wewe kuzama chini zaidi ya kule nuru isiyokoma ya Upatanisho wa Kristo inapong’aa.” Kwa hiyo, katika njia, unaposimama na Kristo, huwezi kushindwa!
Unapotazama kushindwa kwako kama hatua kuelekea mafanikio, unafungua siri ya kutoanguka tena.
Kwa hiyo ijaribu! Na kama utashindwa? Kumbuka tu—wewe hakika hushindwi. Unafanya maendeleo, hatua moja kwa wakati.