Sauti za Vijana
Mwokozi Alinisaidia Kubadilika
Kielelezo na Katelyn Budge
Nina sura hii ambayo, ikiwa sitabasamu, ninaonekana kama nina hasira. Watu wangeuliza, “Kwa nini unanuna? Tatizo lako ni nini?” Na ningesema, “Mimi sijanuna.” Lakini maswali yao kwa kweli yalinikasirisha.
Baba yangu alikuwa na wasiwasi juu yangu. Aliniita chumbani kwake na kusema, “Unajua, huwezi kuendelea kuwa na mtazamo huu wa hasira. Nini kinakusumbua?” Niliamua nilitaka kubadilika.
Nilisali na kumlilia Baba wa Mbinguni anisaidie. Baada ya muda, nilianza kujisikia tofauti. Nimepunguza kidogo kukasirika, ninatabasamu mara kwa mara, na ninawapenda wengine zaidi. Kila mtu alisema, “Unabadilika.” Ninajua kwa kina kwamba siyo kwa nguvu zangu mwenyewe. Ni kwa nguvu inayowezesha ya Upatanisho wa Yesu Kristo.
Ni vigumu kuwa mtu unayetaka uwe. Siwezi bado kusema nimefika ninapotaka kuwa, lakini ninajitahidi kufika huko. Safari yetu inatakiwa kuwa pamoja na Yesu Kristo. Tunapaswa kumwalika Yeye kuwa pamoja nasi.
Victoria E., miaka 16, Lagos, Nigeria
Anapenda kucheza michezo, kusoma, kuimba, kusuka nywele, na kujifunza mambo mapya.