2025
Kwa ajili ya Wakati Unapokuwa Umevunjika Moyo
Machi 2025


Kwa Ajili ya Wakati Unapokuwa Umevunjika Moyo

Mafundisho na Maagano inatoa msaada wakati mambo yanapokuwa hayaendi njia yako.

mkono ukiwa umeshikilia sindano karibu kupasuka kiputo

Kielelezo na Luciana Abrão

Je, umeshawahi kuvunjika moyo? Mimi nimewahi. Kwa kweli, nilivunjika moyo wiki iliyopita. Kweli—machozi na vyote.

Bwana alimwambia Joseph Smith, “Kuwa mvumilivu katika mateso, kwani utapata mengi.” Gugumia. Sipendi sauti ya hilo.

Lakini kwa shukrani, maandiko yanaendelea: “Lakini yavumilie, kwani, lo, Mimi nipo pamoja nawe, hata mwisho wa siku zako (Mafundisho na Maagano 24:8, msisitizo umeongezwa). SAWA. Shusha pumzi ndefu.

Ninapofikiria kuhusu hilo, ninatambua Bwana amekuwa pamoja nami kupitia kila kuvunjika moyo nilikopitia. Hapa kuna baadhi ya mifano:

Wakati Nilipokosa Nafasi …

Nilipokuwa na miaka 15, nilifanya majaribio ya sauti kwa ajili ya mchezo wa kuigiza shuleni. Nilijaribu jukumu la kuongoza, lakini mwishowe, sikupata nafasi hiyo.

Ili kufanya mambo kuwa mabaya zaidi, mwalimu alikuwa tayari amegawa majukumu madogo madogo yote, hivyo hapakuwa na nafasi kwa ajili yangu kabisa. Alinifanya kuwa Kiongozi wa Mwanafunzi, na kwa sababu alijisikia vibaya, aliongeza pia kipengele kipya—nililazimika kuja jukwaani kwa takribani sekunde 30 kama mtawa mkimya.

Ndiyo. Nililia.

… Bwana Aliniimarisha

Nikitazama nyuma, nilitambua Mwokozi alinisaidia kupitia wakati ule wa kuvunjika moyo. Aliniimarisha ili kuweka mtazamo mzuri na kukuza unyenyekevu zaidi. Mwishowe, nilifurahia muda wangu katika mchezo wa daraja la tisa.

“Kwa furaha na tufanye mambo yote yaliyo katika uwezo wetu; na kisha tusimame imara, kwa uhakika mkubwa, kuuona wokovu wa Mungu, na kwa mkono wake kufunuliwa(Mafundisho na Maagano 123:17, msisitizo umeongezwa).

Wakati ambapo Michezo Haikwenda Nilivyotarajia …

Katika mwaka wangu wa mwisho wa shule ya upili, nilitaka kuwa kwenye timu ya chuo kikuu (au timu ya juu) ya tenisi. Ilinibidi nimshinde msichana aliyekuwa juu yangu haraka ili kuwa kwenye timu. Lakini nilipocheza naye, nilipoteza.

Ingawa nilivunjika moyo, nilicheza kwenye timu ndogo ya chuo kikuu. Katika mashindano madogo ya mwisho ya chuo kikuu nilishika nafasi ya kwanza. Lakini unajua nini? Nilipoteza mechi ya mwisho ya fainali. Nililia—tena.

Nilivunjika moyo tena baadaye. Baada ya kupokea tuzo kwa ajili ya kupata alama nzuri na kucheza michezo, waliamua kuchukua tuzo hiyo—kwa sababu ilionekana, ilikuwa tu kwa wale ambao walicheza chuo kikuu.

… Ilikuwa kwa “Wakati Mfupi” tu

Wakati huo, tenisi ilikuwa sehemu kubwa ya maisha yangu, na kuvunjika huko moyo kulionekana kuongezeka. Kile ambacho sikutambua ni kwamba Mwokozi daima alikuwa pamoja nami, akinisaidia. Masikitiko hayo makubwa hayakudumu milele, ingawa ilionekana kuwa hivyo.

Amani iwe katika nafsi yako; Taabu yako na mateso yako yatakuwa kwa muda mfupi; na halafu, kama utastahimili vyema, Mungu atakuinua juu” (Mafundisho na Maagano 121:7–8, msisitizo umeongezwa).

Nilipojaribu Kushinda Kuvunjika Moyo …

Wakati mwingine, nilijaribu kuepuka kabisa kuvunjika moyo. Nilipokuwa na umri wa miaka 13 na sikuweza kuwa kwenye baraza la wanafunzi, sikuwahi kujaribu tena, ingawa ilikuwa ni kitu ambacho labda ningefurahia. Nilikata tamaa kwa sababu nilikuwa na hofu ya kuvunjika moyo tena.

… Nilihitaji “Kutoogopa”

Nilihitaji kukumbuka kwamba Bwana yuko pamoja nasi, hata katika kuvunjika kwetu moyo. Wakati mwingine mambo hayatakwenda tunavyotaka, lakini Anaweza kutusaidia kukabiliana na hisia zisizo na faraja na kujaribu vitu vipya.

“Nitegemeeni katika kila wazo; msitie shaka, msiogope” (Mafundisho na Maagano 6:36–37, msisitizo umeongezwa).

Wakati Natumikia Misioni Haikwenda kama Ilivyopangwa …

Baada ya shule ya upili, niliamua kuhudumu misioni. Lakini nilikuwa na matatizo kadhaa ya kimatibabu ambayo yalinizuia kuondoka wakati nilipotarajia kuondoka.

Ilinibidi niwe mvumilivu, lakini hatimaye niliitwa kwenda Misioni ya Mexico Guadalajara Mashariki. Huko, niliwafundisha watu wengi wa kupendeza na hata kuwasaidia baadhi yao kubatizwa. Lakini hata pamoja na imani yangu, utiifu, na kazi ngumu, hakuna hata mmoja wao aliyeendelea kushiriki kikamilifu Kanisani.

… Nilitumainia katika Mapenzi ya Mungu

Mara nyingi, matukio ya maisha yako nje ya udhibiti wetu. Sikuweza mara moja kutatua matatizo yangu ya kimatibabu. Na siwezi kuwalazimisha wengine kuishi injili. Lakini ninaweza kuamini katika wakati na njia ya Bwana.

“Kwa hiyo, jitakaseni, ili mawazo yenu yawe juu ya Mungu, na siku zitakuja ambazo mtamwona yeye; … nayo itakuwa katika wakati wake mwenyewe, na katika njia yake mwenyewe, na kulingana na mapenzi yake mwenyewe” (Mafundisho na Maagano 88:68, msisitizo umeongezwa).

Wakati Nilipovunjika Moyo Wiki Iliyopita …

Mimi ni mtu mzima sasa. Lakini bado ninavunjika moyo. Kwa kweli, ni wiki iliyopita tu nilikwenda kwenye mkutano wa uandishi. Nilihisi kujiamini sana kuhusu baadhi ya maandishi yangu, lakini nilipokea mrejesho wa kuvunja moyo kutoka kwa waandishi wengine.

… Alikuwa Pamoja Nami

Sasa, ninajaribu kumwamini Bwana zaidi. Kuvunjika moyo ni sehemu ya maisha. Haimaanishi kwamba unafanya jambo lolote lisilo sahihi.

Kwa hiyo, rudi kwenye maandiko kuanzia mwanzo. Ndiyo, tunaweza kuwa na masumbuko na kuvunjika moyo “kwingi.” Lakini najua kwamba Bwana atakuwa pamoja nami kupitia hayo yote. Na Yeye atakuwa pamoja nawe pia.

“Kuwa mvumilivu katika mateso, kwani utapata mengi; lakini utayastahmili, kwani, lo, Mimi nipo pamoja nawe, hata mwisho wa siku zako” (Mafundisho na Maagano 24:8, msisitizo umeongezwa).