Kutumia Mwongozo
Aiskrimu, Urafiki, na Kumpenda Jirani Yako
Kutii amri kuu ya pili si vigumu kama unavyofikiria.
Vielelezo na Valentina Vinci
Wakati rafiki au mwanafamilia anapopitia wakati mgumu sana, je, umewahi kupanga juu ya jinsi ya kufanya matatizo yao yaondoke? Inaonekana kama wazo zuri kwa juu.
Lakini fikiria kwamba wazazi wa rafiki yako wanatalikiana. Au dada yako mdogo anaonewa shuleni. Au babu yako anapambana na msongo mkali wa mawazo. Je unashughulikiaje yote hayo?
Jibu fupi ni huwezi. Na hiyo ni sawa. Wakati huo huo, bado unaweza siku zote kusaidia. Na utashangazwa ni kiasi gani kidogo cha msaada kinaweza kugeuza mambo.
Mapambano Makubwa, Ukarimu Rahisi
Foni P. alikulia katika nyumba ya mzazi mmoja. Wakati wa utoto wake na miaka ya ujana, Foni alitazama mapambano ya mama yake ya kuwalea watoto watatu peke yake. Matokeo yake, Foni alikuza hisia hasi kwa baba yake. Kisha hivi karibuni, baada ya kufikisha umri wa miaka 19, baba yake alianza kujaribu ili kuwafikia na kuungana.
“Nilikasirishwa,” Foni anasema. “Fikra zangu zilikuwa, ‘Alikuwa na miaka 19 ya kuingia maishani mwangu lakini hakufanya hivyo. Kwa nini sasa?’” Japokuwa alisali na kutafakari, Foni bado hakuweza kupata amani. Kuzungumza na mama yake na shangazi yake kulimsaidia kidogo, lakini bado ilimwacha akihisi amefungwa kwa mafundo. Kisha kitu cha ajabu (lakini rahisi) kilitokea: Rafiki kipenzi wa Foni alimwalika watoke kwa ajili ya aiskrimu na kufanya manunuzi.
“Watu wengi wangeangalia hilo na kufikiri haikuwa jambo kubwa,” Foni anasema, “lakini ilimaanisha mengi sana! Nilihisi jua kwenye ngozi yangu. Tulikuwa tukitembea nje, na nikaona miti. Nilihisi upepo, na nilimhisi Roho wakati huo huo. Ilikuwa ya kustaajabisha.”
Je, safari hii ya ghafla ya manunuzi ilitatua matatizo ya Foni? Hapana. Foni anakiri kwamba uhusiano wake na baba yake bado ni changamoto. Lakini kitendo hicho rahisi cha ukarimu kutoka kwa rafiki yake kilimruhusu Foni kumhisi Roho Mtakatifu tena. Kisha angeweza kukabiliana na mapambano yake kwa nguvu za ziada. “Ninajua alishawishiwa na Roho Mtakatifu kunitoa nje ya nyumba,” Foni anashiriki.
Nani Anakuhitaji Wewe Leo?
Katika mwongozo wa Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana , tunaalikwa “kuwafikia wale wanaojisikia wapweke, waliotengwa, au wasiojiweza. Wasaidie wauhisi upendo wa Baba wa Mbinguni kupitia wewe” (Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana: Mwongozo kwa ajili ya Kufanya Chaguzi [2022], 12). Kitendo hicho rahisi cha urafiki kilimsaidia Foni kuhisi upendo wa Mungu wakati wa hali ngumu. Je, ni nani unaweza kumsaidia ahisi upendo kama huo leo?