2025
Ninawezaje bado kuwa na tumaini na kujiandaa kwa ajili ya familia yangu ya baadaye wakati ulimwengu unakatisha sana tamaa?
Machi 2025


Maswali na Majibu

“Ninawezaje bado kuwa na tumaini na kujiandaa kwa ajili ya familia yangu ya baadaye wakati ulimwengu unakatisha sana tamaa?”

msichana

“Bwana ametuamuru sisi kuongezeka na kuijaza dunia na kuahidi kutulinda kupitia maagano tuliyofanya na Yeye. Mpango wa Mungu ni mkamilifu. Ninajua kwamba ninapokuwa na watoto—kama ninatii kile alichoniamuru—Yeye analazimika kunibariki na kunilinda mimi na familia yangu kulingana na hekima Yake.”

Ziona O., 16, Hawaii, Marekani

mvulana

“Ninapata tumaini ninapotumia imani katika Mungu na mpango Wake kwa ajili yangu. Wakati ulimwengu unapokatisha tamaa, ninaweza kumgeukia Yeye kwa ajili ya amani. Baraka yangu ya kipatriaki inanisaidia kujua kwamba Baba yangu wa Mbinguni ananijua vizuri zaidi kuliko mtu yeyote na kwamba ananipenda. Inanipa kujiamini kwamba kila kitu kitafanikiwa.”

Logan A., 16, Texas, Marekani

msichana

“Inasaidia kwa mimi kujua kwamba Mungu ananipenda, ana mpango kwa ajili yangu, na atanisaidia katika nyakati ngumu. Pia inasaidia kujua kwamba maagano yangu yananiunganisha kwa Kristo na kunipa fursa ya kufikia uweza na nguvu Zake.”

Lydie L., 18, Utah, Marekani

mvulana

“Pata shangwe katika Kristo, maandiko, na sala. Kama tunaweza kujifunza kwamba maoni pekee ambayo ni muhimu ni maoni ya Mwokozi, itafanya maisha kuwa rahisi zaidi. Kufanya maamuzi kulingana na maoni ya watu wanaotuzunguka kunaweza kutulazimisha kufanya maamuzi hasi.”

Lily W., 16, Utah, Marekani

msichana

“Tunapaswa kuweka tumaini letu kwa Mungu na kukuza mawazo chanya. Tunaweza kupata mwongozo wa kiungu kutoka kwa wengine ambao wameshinda changamoto kama hizo. Pia, kushika amri, hususani sheria ya usafi wa kimwili na kuwa na utu wema, huweka msingi imara wa kujenga maisha ya familia yenye kuridhisha licha ya kuvunjika moyo kwa nje.”

Mungu O., 19, Lagos, Nigeria