“Adamu na Hawa,” Rafiki, Januari 2026, 46–48.
Njoo, Unifuate
Adamu na Hawa
Adamu na Hawa walikuwa watoto wa kwanza wa Baba wa Mbinguni kuishi duniani. Waliishi katika Bustani ya Edeni.
Mungu aliwaacha wale matunda ya kila mti isipokuwa mmoja. Ikiwa wangekula kutoka mti wa ujuzi wa mema na mabaya, wangepaswa kuondoka bustanini na hatimaye wangekufa. Lakini Shetani aliwadanganya. Alisema ikiwa wangekula tunda, wangejua mema na mabaya lakini hawangekufa.
Hawa alichagua kula tunda.
Kisha alimpa Adamu sehemu ya tunda. Adamu pia alichagua kula tunda.
Mungu na Yesu Kristo waliwatembelea, lakini Adamu na Hawa waliogopa na walijificha. Mungu aliuliza kama walikuwa wamekula tunda kutoka kwenye ule mti.
Adamu na Hawa walisema kwamba walikula tunda. Sasa iliwabidi kuondoka kutoka kwenye Bustani ya Edeni. Lakini Mungu alikuwa na mpango kwa ajili yao. Sasa walijua mema na mabaya na wangeweza kupata watoto
Adamu na Hawa waliahidi kutii amri za Mungu. Walijifunza zaidi kuhusu Mwana wa Mungu, Yesu Kristo. Walihisi shangwe kubwa kwa sababu Yeye angeisaidia familia yao kurudi kwa Mungu.