“Thomas Mkusanyaji,” Rafiki, Januari 2026, 17.
Thomas Mkusanyaji
Jina langu ni Thomas, na mimi ni mkusanyaji.
Mwaka huu katika Msingi tunajifunza jinsi ya kukusanya. Viongozi wetu walituomba tukusanye familia zetu kwa ajili ya sala na kujifunza maandiko. Wanatutaka tufanye mazoezi ya kukusanya ili tujue jinsi ya kukusanya sasa na wakati tunapokua—kwenye misheni, shuleni, au hata wakati tuko peke yetu. Kwa njia hiyo tunaweza daima kukusanyika kiroho pamoja na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo na kupata amani katika Wao.
Kazi yangu ni kuikusanya familia yangu kwa ajili ya sala ya asubuhi. Ninauliza, “Tafadhali utaungana nami kwa ajili ya sala?” Kaka yangu Henry anatukusanya kwa ajili ya sala ya jioni na kujifunza maandiko.
Jumamosi moja asubuhi, tuliondoka mapema kucheza mpira wa kikapu. Baadaye, tulienda kufanya kazi. Ghafla nilikumbuka na kusema, “Mama, tulisahau kukusanyika kusali.” Aliniambia tungeweza kukusanyika tulipofika nyumbani. Lakini nilisema, “Tunahitaji kukusanyika na kusali sasa hivi!” Aliniomba nisali, lakini aliweka macho yake wazi kwa sababu alikuwa anaendesha gari.
Mama na Baba wanamuambia Henry na mimi jinsi walivyo na shukrani kwamba tunaikusanya familia yetu kwa ajili ya sala na kujifunza maandiko. Wanasema sauti zetu ndogo zinaleta tofauti kubwa katika nyumba yetu. Wanatuambia kwamba kwa sababu tunakusanyika, familia yetu imebarikiwa.
Vielelezo na Augusto Zambonato