Rafiki
Mwanzo Mpya
Januari 2026 Rafiki


“Mwanzo Mpya,” Rafiki, Januari 2026, 38–39.

Mwanzo Mpya

“Ninawezaje kuwa msafi baada ya kubatizwa?”

Hadithi ya kweli kutoka Ufaransa.

Kielelezo cha mvulana mdogo na baba yake wakishikana mikono na kutembea nje

Alexandre angekuwa umri wa miaka minane katika siku chache tu! Alikuwa na furaha sana kwa sababu yeye na Baba walikuwa wanapanga asusa maalum ya siku ya kuzaliwa kwa ajili yake kula baada ya shule. Wamisionari walipowasili kwa ajili ya chakula cha jioni, Alexandre aliwaambia wote kuhusu keki za chokoleti tamu alizozichagua.

“Tutakuwa na nane kati yazo na mshumaa mmoja kila mmoja, badala ya keki moja yenye mishumaa minane!”

Mzee Lauener alicheka. “Hiyo inaonekana vizuri sana! Hifadhi baadhi kwa ajili yangu!”

Baada ya chakula cha jioni, wamisionari walifundisha somo juu ya ubatizo. Mzee Doyon alimgeukia Alexandre. “Wakati unapobatizwa, unaahidi kumfuata Yesu Kristo.” Alimwambia Alexandre kuhusu ubatizo wake mwenyewe na kushiriki ushuhuda wake. “Roho Mtakatifu alinisaidia kuhisi furaha sana kwa sababu siku hiyo nilichagua kumfuata Yesu Kristo.”

Alexandre hakuweza kusubiri siku yake ya ubatizo!

Lakini alipokwenda kulala usiku ule, alipata ikiwa vigumu kulala. Alipenda wazo la kuwa msafi na mpya. Lakini ni kwa jinsi gani angebaki msafi baada ya ubatizo?

Asubuhi iliyofuata Alexandre alitembea kwenda shuleni pamoja na Baba. “Kwa kweli umekuwa kimya asubuhi ya leo,” Baba alisema. “Kuna nini?”

Alexandre alipumua. “Mini natamani ningeweza kubatizwa zaidi ya mara moja.”

“Kwa nini?” Baba aliuliza.

“Ni kwa njia gani ingine nitabaki kuwa msafi baada ya kubatizwa?” aliuliza Alexandre. “Mimi usahau mambo wakati wote—kama kusema jambo na asante kwa wakubwa na kuwa mvumilivu na kaka mdogo wangu. Ninajua bado nitafanya makosa. Unapata ubatizo mmoja tu, kwa hiyo kamwe sitaweza kuwa msafi tena.”

Baba alisimama na kukutana na macho ya Alexandre. “Wee! Hiyo labda inahisi kuzidiwa kidogo. Je, unakumbuka wakati tulipozungumza kuhusu kufanya ahadi wakati wa ubatizo?”

Alexandre aliitikia kwa kichwa. “Nadhani hivyo.”

“Unapobatizwa, unafanya agano na Baba wa Mbinguni. Unaahidi kutii amri Zake na kumfuata Yesu Kristo. Baada ya hapo, kila wakati unapopokea sakramenti, unaweza kumkumbuka Yesu na jinsi Yeye anavyoweza kukusaidia kutubu.”

Macho ya Alexandre yalitanuka. “Kwa hiyo ninaweza kuhisi msafi kama wakati ninapobatizwa?”

“Kabisa,” Baba alisema. “Baba wa Mbinguni anajua wewe si mkamilifu, na wakati mwingine utafanya chaguzi mbaya. Lakini unapotenda dhambi, unaweza kutubu na kuendelea kujaribu kumfuata Yesu. Je, hilo linasikika kama kitu unachoweza kufanya?”

Alexandre alitabasamu. “Ndiyo! Nafikiria naweza kufanya hivyo.”

Wakati siku ya kuzaliwa ya Alexandre ilipowasili, familia yake ilipata asusa ya siku ya kuzaliwa baada ya shule. “Ilikuwa tamu sana!” Na kwenye ubatizo wake, Alexandre alihisi vizuri zaidi ndani wakati alipotoka nje ya maji. Alikuwa ameahidi kumfuata Yesu Kristo, na hiyo ilionekana ya kushangaza!

Mvulana akila keki za chokoleti

Wiki hiyo Alexandre alijaribu kwa uwezo wake wote kuweka maagano yake mapya na kuwa mkarimu kwa kaka yake mdogo. Lakini Jumapili iliyofuata ilipofika, alikatishwa tamaa kidogo. Alihisi kama angefanya chaguzi nzuri zaidi wiki hiyo.

Wakati sakramenti ilipokuwa ikipitishwa, Alexandre alikunja mikono yake na kusujudu kichwa chake. Kimya kimya alimsihi Baba wa Mbinguni amsaidie afanye vizuri zaidi wiki ijayo. Alifikiria ni kiasi gani Yesu alimpenda na jinsi alivyotaka kuwa zaidi kama Yeye.

Alipokuwa akichukua kipande cha mkate kutoka kwenye trei ya sakramenti, Alexandre alihisi ukunjufu na amani ndani yake. Alihisi kama alivyokuwa katika siku yake ya ubatizo! Baba aliweka mkono wake kuzunguka bega la Alexandre na kumpa tabasamu.

Leo ilikuwa mwanzo wa wiki mpya, na Alexandre alikuwa anaenda kufanya kadiri awezavyo—kwa msaada wa Baba wa Mbinguni.

Mvulana akipokea sakramenti
Maandishi mbadala

Vielelezo na Toby Newsome