“Mpango wa Furaha na Wewe!” Rafiki, Januari 2026, 24–25.
Mpango wa Furaha na Wewe!
Baba wa Mbinguni alitengeneza mpango kwa ajili ya watoto Wake wote unaoitwa mpango wa furaha. Wewe una sehemu katika mpango huo!
Uumbaji
Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo waliumba mbingu na nchi na kila kitu kilicho ndani yake.
Anguko
Adamu na Hawa walichagua kula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Kwa sababu ya hili, walitenganishwa na Mungu, walijua mema na mabaya, na wangeweza kuwa na familia. Wao walikuwa familia ya kwanza duniani.
Upatanisho wa Yesu Kristo
Yesu Kristo alikuja duniani. Yesu Kristo aliusikia uchungu wetu wote na alilipia dhambi zetu. Yeye alikufa na kuishi tena. Kwa sababu Yake, tunaweza kutubu na kuishi na familia zetu na Baba wa Mbinguni tena siku moja.
Maisha Duniani
Sote tulizaliwa duniani ili kupokea mwili, kujifunza na kukua. Tunaweza kumfuata Yesu Kristo kwa kutii amri na kuwatumikia wengine.
Je, unaweza kupata vitu hivi katika picha?
Vielelezo na Maddie Baker