“Ziko Wapi Baraka Zangu Nilizoahidiwa kutokana na Kulipa Zaka?,” Liahona, Sept. 2025
Ziko Wapi Baraka Zangu Nilizoahidiwa kutokana na Kulipa Zaka?
Baba wa Mbinguni mara nyingi hutupa baraka “muhimu lakini ngumu kuelezea” badala ya miujiza ya haraka wakati tunapolipa zaka yetu.
Kielelezo na Dilleen Marsh
Malaki alitabiri kwamba kama tutalipa zaka zetu kwa Mungu, kisha Yeye atafungua madirisha ya mbinguni, na kumwaga baraka, “kwamba hapatakuwa na nafasi ya kutosha kuhifadhi.” (Malaki 3:10).
Kwa ahadi hiyo, mara nyingi tunasikia hadithi za baraka za kimiujiza na za papo hapo ambazo zilikuja kwa wale walioheshimu amri ya kulipa zaka zao. Lakini nini hutokea kama hatupokei baraka kama hizo katika nyakati zetu za mahitaji ya muda? Kutoona baraka kama hizo kunakuja kutimizwa katika maisha yetu wenyewe kunaweza kuvuruga moyo. Tunaweza hata kuuliza, “Je, mimi sijabarikiwa?”
Mzee Neil L. Andersen wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili anatukumbusha kwamba “madirisha ya mbinguni hufunguka katika njia nyingi. Baadhi ni za kimwili, lakini nyingi ni za kiroho. Baadhi ni ndogo na rahisi kupuuzwa. Kutumaini katika ratiba ya Bwana; baraka daima zinakuja.”
Mafundisho kutoka kwa Mzee David A. Bednar wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili yanaweza pia kutusaidia kuona kwamba baraka tunazopokea zinaweza kuja kwa njia nyingi ambazo hatuwezi kuzingatia. Alisema, “Baadhi ya baraka tofauti tofauti tunazopokea tunapokuwa watiifu kwa amri hii [sheria ya zaka] ni muhimu na ni ngumu kuelezea. Baraka kama hizo zinaweza kutambulika kama sisi tu wasikivu kiroho na tuko macho (ona 1 Wakorintho 2:14).”
Kutazamia na kutambua baraka muhimu zilizo ngumu kuelezeka za kulipa zaka kamili kunaweza kutusaidia kuelewa kwamba Mungu anatujua sisi na anatubariki.
Baraka Muhimu lakini Ngumu Kuelezeka
Mapenzi ya Mungu daima si sawa na yetu (ona Isaya 55:8–9). Kwa sababu hiyo, baraka za Mungu zinaweza daima zisije kwetu katika njia tunayotamani au kutarajia. Kwa mfano, Mzee Bednar alitoa baadhi ya mifano ya baraka zisizotarajiwa ambazo zinaweza kuja kutokana na kulipa zaka: “Wakati mwingine tunaweza kumwomba Mungu mafanikio, na Yeye hutupa ushupavu wa kimwili na kiakili. Tunaweza kusihi tupate ustawi, na tupokee mtazamo mkubwa na ongezeko la uvumilivu, au tunaomba tupate ukuaji na tunabarikiwa na kipawa cha neema. Yeye anaweza kututunukia sisi na msimamo na imani tunavyojitahidi kupata malengo yanayostahili. Na tunaposihi tupate msaada kutokana na ugumu wa kimwili, kiakili, na kiroho, Yeye anaweza kuongezea azma na uthabiti.”
Mzee Bednar pia alipendekeza kwamba wakati mwingine “baraka ambazo huja kwetu kupitia kwa madirisha ya mbinguni inaweza kuwa uwezo mkubwa wa kutenda na kubadilisha hali zetu wenyewe badala ya kutarajia hali zetu kubadishwa na mtu au kitu kingine.” Ona, kwa mfano, jinsi mume na mke kutoka Argentina walivyohisi hivi katika maisha yao katika hadithi yao “Kwa Nini Bado Unalipa Zaka?” (Liahona, Machi 2013, 37).
Wakati wa Mungu
Tunaweza pia kujifunza kutumainia kwamba baraka huja katika wakati wa Mungu mwenyewe na katika njia Yake mwenyewe.
Mzee Michael John U. Teh wa Wale Sabini alisema: “Tunapotii sheria ya zaka, sisi … haipaswi kumpa Bwana tarehe ya mwisho. Kuna mwelekeo kwa baadhi kutarajia baraka za mali kuja wakati fulani wa makadirio yao wenyewe. Hivi ndivyo wengi wanavyopoteza ujasiri wao katika ahadi Zake. Wao ni waaminifu mwanzoni lakini kisha wanaacha kutii baada ya muda fulani wakati matarajio yao hayafikiwi. Tunahitaji kutambua kwamba mambo yote yanafanyika kulingana na mapenzi na ratiba ya Bwana na si yetu.”
Kuelewa kwamba ratiba ya Mungu ni tofauti na yetu kunaweza kutusaidia kutambua vyema zaidi kwamba kwa sababu tu hatujapata muujiza wa haraka, haimaanishi kwamba hatujabarikiwa.
Hekima ya Mungu
Rais Dallin H. Oaks, Mshauri wa Kwanza katika Urais wa Kwanza, alifundisha: “Mtu fulani amesema kwamba maisha ni kile kinachotutokea wakati tunapofanya mipango mingine. Kwa sababu ya vitu ambavyo hatuna udhibiti, hatuwezi kupanga na kuleta kila kitu tunachotamani katika maisha yetu. Mambo mengi muhimu yatatokea katika maisha yetu ambayo hatujapanga, na siyo yote yatakaribishwa.”
Katika safari yetu duniani, hata wale ambao ni watiifu kwa sheria ya zaka wanaweza kupata uzoefu wa mapambano ya kifedha ya ukosefu wa ajira, dharura zisizotarajiwa, ubadhirifu wa fedha, au mshahara kudoda. Kujua kwamba Mungu yuko katika udhibiti kunaweza kutusaidia kukua katika imani na subira tunapotafuta baraka muhimu na ngumu kuelezea za zaka. Inaweza kuwa kwamba baadhi ya matatizo haya kwa kweli ni baraka ambazo zitatusaidia kukua kupitia majaribu yenyewe.
Mzee Hugh B. Brown wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili (1883–1975) wakati mmoja alishiriki somo kama hilo alilojifunza wakati akipogoa kichaka cha currant kwenye shamba huko Kanada.
Alipokwenda kusafisha na kurekebisha shamba lake, alipata kichaka cha currant ambacho kilikuwa kimekua zaidi ya futi sita juu na hakikuwa na matunda. Kwa hiyo, aliipogoa kwa kiasi kikubwa, na kuacha tu visiki vidogo, vyenye umbo la chozi. Uoni ulionekana kana kwamba kichaka cha currant kilikuwa kikilia, na Mzee Brown alidhani alisikia kichaka kikisema:
“Ni kwa jinsi gani ungeweza kufanya hili kwangu? Nilikuwa nikikuza ukuaji wa ajabu kama huo. … Na sasa umenikata chini. … Nilidhani wewe ni mtunza bustani hapa.”
Mzee Brown alijibu, “Angalia, kichaka kidogo cha currant, mimi ni mtunza bustani hapa, na ninajua ninachotaka wewe uwe. Ikiwa nitakuacha uende jinsi unavyotaka kwenda, huwezi kamwe kuwa kitu chochote. Lakini siku moja, unapokuwa umelemewa na matunda, utafikiria nyuma na kusema, ‘Asante, Bw. Mtunza bustani, kwa kunikata chini, kwa kunipenda vya kutosha kuniumiza.’”
Tunapopambana kifedha na hatuoni baraka zilizoahidiwa za kulipa zaka, tunaweza kwa machozi kumuuliza Mungu kwa njia sawa na hiyo, “Unawezaje kufanya hivi kwangu? Ninafanya yote ambayo umeomba. Na sasa umenikatia chini.”
Katika nyakati hizi, tunaweza kuchukua muda kufikiria kama majaribu tunayopitia kwa kweli yataleta baraka kubwa kutokana na masomo tunayojifunza katika safari hii. Tunaweza kujifunza kumtumainia kikamilifu Mtunza Bustani na baraka Yeye alizoziweka kwa ajili yetu tunapobaki karibu Naye.
Tumaini Endelevu na Sala
Baraka zilizo ngumu kuelezea lakini muhimu ambazo Mungu hutupatia kutokana na kulipa zaka zinaweza kutusaidia kuinuka juu ya matatizo mengi ya ulimwengu. Baba yetu mpendwa wa Mbinguni atatengeneza kikamilifu baraka hizi ili kutusaidia kukua na kuwa zaidi kama Yeye. Tunapofanyia mazoezi imani katika kutambua na kukubali baraka zote zinazokuja, tunaweza kuona utimilifu wa ahadi ya Malaki.
Tunapokuwa na shaka na kukata tamaa kutokana na mapambano ya kifedha, kama kwa machozi tunatilia shaka kama tumebarikiwa, hatukati tamaa ya tumaini! Badala yake, tunaweza kuomba ili kuona baraka ngumu kuelezea na muhimu ambazo Bwana ametupatia na kuwa na imani katika mpango wa Baba wa Mbinguni kwa ajili yetu.
Kama Mzee Andersen alivyoshuhudia, “Ninawaahidi kwamba mnapomwamini Bwana, baraka za mbinguni zitafuata.”