2025
Kwa Usanifu wa Kiungu: Mafundisho ya Kitume juu ya Familia
Septemba 2025


“Kwa Usanifu wa Kiungu: Mafundisho ya Kitume juu ya Familia,” Liahona, Sept. 2025.

Kwa Usanifu wa Kiungu: Mafundisho ya Kitume juu ya Familia

Kama wana na mabinti wa Mungu, sisi sote ni washiriki wa familia ya mbinguni ambayo inatoa mfano kwa familia zetu duniani.

Picha rasmi Urais wa Kwanza 2018

“Bwana ameiteua familia kuwa kitengo cha msingi cha Kanisa na jamii.” Familia zinaweza kuwa na mume na mke pamoja na watoto, na zinaweza pia kuwa mtu mmoja, mzazi mmoja na watoto, au mume na mke bila watoto. Na wakati mwingine familia hizi zinaweza kuwajumuisha ndugu wengine. Bila kujali hali yetu ya kindoa au hali ya mtu binafsi, kila mmoja wetu ni wa sehemu ya familia ya Mungu, kila mmoja wetu ni mshiriki wa familia duniani, na sisi kila mmoja wetu anajitayarisha kuwa wazazi wa milele.

Kwa milenia, manabii na mitume wametangaza utakatifu wa familia na kuonya juu ya majanga yatakayowapata watu binafsi, mataifa na ulimwengu kama familia hazitahifadhiwa na kulindwa. Haya ni baadhi ya maneno ya kuvutia kutoka kwa manabii na mitume kuhusu familia na umuhimu wa “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu.”