Maswali na Majibu
“Marafiki zangu wema wanafanya chaguzi ambazo zinanifanya kutojisikia vizuri. Nifanye nini?
“Zungumza na rafiki zako kuhusu hisia zako. Njia ya uhusiano wenye afya hufunguka wakati tunapowasiliana. Wakati mwingine ni vigumu kwa sababu tunafikiri marafiki zetu wanaweza kukasirika, lakini kuna suluhisho: fanya kile ambacho Kristo angefanya na kutenda kwa huruma.”
Luan R., 19, São Paulo, Brazili
“Wakati mwingine marafiki hufanya chaguzi kwa sababu ya shinikizo la rika. Kama nitazungumza na rafiki zangu kuhusu chaguzi zao, ninaweza kuwasaidia kuwajibika kwenye malengo na maadili yao. Wakati mwingine, hatukubaliani na kile kilicho kizuri au muhimu, lakini lazima tuheshimu maoni na haki ya kujiamulia ya kila mmoja wetu.”
Maggie J., 18, Texas, Marekani
“Pengine unajisikia vibaya kwa sababu Roho Mtakatifu anakuambia kwamba kile wanachofanya si sahihi. Waalike kufanya kitu kingine.”
Lorenzo M., 12, Quezon City, Ufilipino
“Ungeweza kuwaongoza kuelekea njia ya Mungu au pata marafiki wengine ambao watakuwa ushawishi mzuri. Sali ili kujua uamuzi wa kufanya. Amini uamuzi wa Baba yako wa Mbinguni, na Yeye atakuongoza.”
Haiden W., 15, Washington, Marekani
“Ningefanya kadiri niwezavyo kuwa mfano mzuri. Pia ningesali kwa ajili yao kwa sababu ninajua kwamba nuru daima inaishinda giza.
Isaac M., 19, Lualaba, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
“Kuwa imara na jasiri kama vile Moroni alivyokuwa. Sote hatimaye tutakuwa na marafiki wakifanya maamuzi mabaya, na tutahitaji msaada kutoka kwa Baba wa Mbinguni ili kuvuka. Kila asubuhi ninasali ili kuvaa silaha za Mungu, na hii inanisaidia sana!”
Asa F., 15, Utah, Marekani
“Wapende na uache nuru yako iangaze. Watu wataanza kuheshimu maamuzi yako. Mimi na familia yangu tulikuwa waumini pekee wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho katika shule yetu, na niligundua kwamba watu waliacha kuapa tukiwepo kwa sababu walijua tulikuwa tofauti.”
Penelope W., 13, Mkoa wa Kati, Ureno