2025
Je, Ni Nini Kinafanya Kanisa Lako Kuwa Tofauti?
Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Septemba 2025


“Je, Ni Nini Kinafanya Kanisa Lako Kuwa Tofauti?”

Tamara W. Runia

Nilizoea kujiuliza ningesema nini kama mtu angeuliza, “Ni nini kinafanya kanisa lako liwe tofauti?” Kisha mwana wetu mkubwa alikufa bila kutarajia, akimwacha nyuma mke wake mzuri na watoto wanne. Katika huzuni yetu, mafundisho ya injili ya Yesu Kristo iliyorejeshwa yalileta uwazi na faraja. Toleo la mwezi huu linaangazia mafundisho matatu ya kipekee:

Kwanza, tangazo lenye mwongozo wa kiungu la familia linafundisha kwamba “mpango mtakatifu wa furaha unawezesha uhusiano wa familia kuendelezwa zaidi ya kaburi. (Ona ukurasa wa 26.)

Pili, kupitia Kanisa la Bwana, tuna fursa ya kufikia mamlaka na nguvu ya ukuhani wa Mungu—nguvu ile ile ambayo iliumba dunia na inaziunganisha familia milele. (Ona ukurasa wa 2.)

Tatu, watu wa agano wa Mwokozi katika Kanisa Lake wanajitayarisha kwa ajili ya Ujio Wake wa Pili, ambao ni sababu ya shangwe. Ona ukurasa wa 18, 22

Unapojifunza toleo hili, naomba ugundue kweli hizi wewe mwenyewe na kupata majibu yako kwa swali, “Je, Ni Nini Kinafanya Kanisa Lako Kuwa Tofauti?”

Rafiki yako,

Tamara W. Runia

Mshauri wa Kwanza katika Urais Mkuu wa Wasichana