2025
Msongo wa Mawazo, Roho, na Maandiko
Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Septemba 2025


Sauti za Vijana

Msongo wa Mawazo, Roho, na Maandiko

msichana

Kielelezo na Katelyn Budge

Nimehama hama sana katika maisha yangu. Miaka michache iliyopita, tulihamia Dubai kwa muda mfupi. Nilipofungua sanduku langu, kitu cha mwisho chini kilikuwa maandiko yangu. Nilifikiria kwamba nilipaswa kuyasoma. Nilifanya hivyo, kitu ambacho si cha kawaida kwa sababu mimi daima si mzuri katika kufuatilia misukumo. Lakini nilianza mwanzo kabisa, na nadhani nilisoma sura tano au sita.

Baadaye, niliombwa kuzungumza kanisani. Nilivutiwa kuzungumza kuhusu umuhimu wa kujifunza maandiko. Niliandika hotuba yangu na nikawaza, “Wow, ninapaswa kusoma zaidi maandiko.” Pia ilikuwa kana kwamba kulikuwa na ushindani kati yangu na baba yangu. Alikuwa katika Alma, na nilitaka kumfikia. Nilianza kusoma maandiko yangu kila siku—wakati mwingine sura 10 au 15!

Nilianza kutambua matukio mengi zaidi ya kiroho. Unaposoma mengi kiasi hicho, inakupa nafasi ya kuwa na ufunuo binafsi. Hakika nilikuwa nikitenga muda kwa ajili ya Bwana.

Nilianza kutunza shajara ya kiroho. Katika ingizo moja, niliandika, “Nilikuwa nikisoma 3 Nefi kuhusu jinsi Yesu Kristo alivyoshuka chini kwa watu na mambo yote ya kupendeza aliyoyafanya. Nilihisi kuwa karibu sana na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo leo.”

Hakika nilishangazwa sana ni uzoefu kiasi gani niliokuwa nao, hasa nilipokuwa nikiutafuta. Nilisema, “Wow, Mungu kweli anazungumza sana na mimi.”

Kujifunza maandiko kulinisaidia sana, hasa kwa msongo wote wa mawazo uliotokana na kuhama hama sana. Maandiko ni maneno ya Kristo. Yeye huzungumza nasi kupitia hayo. Kupitia maneno Yake, ninaweza kusogea karibu Naye.

msichana

Linnaea E., umri miaka 16, Hawaii, Marekani

Anapenda kucheza tenisi, kupanda milima, kuteleza katika mawimbi meupe kwa ubao, na kupiga kinanda.