72
Je, Uliomba?
Kwa kutafakari
1. Ulipoamka leo,
Je, uliomba?
Katika jina la Kristo,
Kusihi upendeleo
Ili kulindwa?
[Chorus]
Jinsi sala hufariji!
Nuru huongezeka.
Punde ukiwa gizani,
Kumbuka sala.
2. Ulipopata hasira,
Je, uliomba?
Upewe neema, ndugu,
Wengine usihukumu,
Waliokosa?
[Chorus]
Jinsi sala hufariji!
Nuru huongezeka.
Punde ukiwa gizani,
Kumbuka sala.
3. Ulipopatwa na shida,
Je, uliomba?
Ulipojawa huzuni,
Malhamu ya Gileadi
Ulitafuta?
[Chorus]
Jinsi sala hufariji!
Nuru huongezeka.
Punde ukiwa gizani,
Kumbuka sala.
Maandishi: Mary A. Pepper Kidder, 1820–1905
Muziki: William O. Perkins, 1831–1902
Zaburi 5:3, 12
Marko 11:24–25