112
Mwokozi Amefufuka
Kwa shangwe
1. Mwokozi amefufuka, Haleluya!
Tuseme na malaika, Haleluya!
Ushindi kwake juu, Haleluya!
Imba dunia na mbingu, Haleluya!
2. Ukombozi ameleta, Haleluya!
Na vita amevishinda, Haleluya!
Yesu hana mateso, Haleluya!
Na giza tena haliko, Haleluya!
3. Kristo tena anaishi, Haleluya!
Nguvu ya kifo i wapi? Haleluya!
Afa kutuokoa, Haleluya!
Kaburi u wapi sasa? Haleluya!
Maandishi: Charles Wesley, 1707–1788
Muziki: Hajulikani, Lyra Davidica, 1708
Mathayo 28:5–6
1 Wakorintho 15:20, 53–57