Sura ya 6
Kuwasilishwa Hekaluni
Yesu alipokuwa na umri wa wiki chache, wazazi Wake walimleta Yerusalemu ili kumwasilisha hekaluni.
Luka 2:22
Simeoni, mtu mwenye haki aliyeishi Yerusalemu, alikuwa hekaluni. Roho Mtakatifu alimwambia angemwona Kristo kabla hajafa.
Luka 2:25–26
Simeoni alimwona mtoto Yesu hekaluni. Alimbeba mikononi mwake na kumsifu Mungu.
Luka 2:27–29
Simeoni alisema kwamba mtoto huyo angeleta wokovu kwa watu wote. Yusufu na Mariamu walistaajabu kwa yale aliyosema.
Luka 2:30–33
Mjane aliyeitwa Ana pia alimwona Yesu na alijua Yeye alikuwa nani. Alitoa shukrani na kuwaambia watu wengi kuhusu Yeye.
Luka 2:36–38