Hadithi za Maandiko
Sura ya 6: Kuwasilishwa Hekaluni


Sura ya 6

Kuwasilishwa Hekaluni

Yusufu, Mariamu, na mtoto Yesu hekaluni

Yesu alipokuwa na umri wa wiki chache, wazazi Wake walimleta Yerusalemu ili kumwasilisha hekaluni.

Luka 2:22

Simeoni akiota ndoto juu ya Yesu Kristo

Simeoni, mtu mwenye haki aliyeishi Yerusalemu, alikuwa hekaluni. Roho Mtakatifu alimwambia angemwona Kristo kabla hajafa.

Luka 2:25–26

Simeoni akiwa amembeba mtoto Yesu

Simeoni alimwona mtoto Yesu hekaluni. Alimbeba mikononi mwake na kumsifu Mungu.

Luka 2:27–29

Simeoni akiwa amembeba mtoto Yesu

Simeoni alisema kwamba mtoto huyo angeleta wokovu kwa watu wote. Yusufu na Mariamu walistaajabu kwa yale aliyosema.

Luka 2:30–33

Ana akimuona mtoto Yesu

Mjane aliyeitwa Ana pia alimwona Yesu na alijua Yeye alikuwa nani. Alitoa shukrani na kuwaambia watu wengi kuhusu Yeye.

Luka 2:36–38